• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI SIKU YA WAUGUZI DUNIANI

Tarehe ya kuwekwa: May 13th, 2023

Siku ya wauguzi Duniani ( International Nurse Day) huadhimishwa ulimwenguni kote kila mwaka tarehe 12 Mei wakikumbuka na kutafakari mchango wao wanaotoa kwa jamii.

Siku hiyo iliibuliwa kwa mara ya kwanza  mwaka 1953 na Dorothy Sutherland aliyekuwa Afisa kutoka kitengo cha Elimu ya Afya na Ustawi Nchini U.S kwa lengo la kuangalia mchango wa Wauguzi katika kuhudumu jamii.

Baraza la Wauguzi Ulimwenguni (International Council of Nurse) ilianza kuadhimisha siku hiyo tangu mwaka 1965 na mwaka 1974 Januari ambapo ilitolewa tamko rasmi kuwa Siku ya Wauguzi Duniani iadhimishwa Ulimwenguni kote tarehe 12 Mei.

Hayo yalibainishwa kwenye sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani iliyofanyika kiwilaya katika Viwanja vya Mjimwema Kituo cha Afya na kuhudhuriwa na Wauguzi, pamoja na wadau mbalimbali wa afya.

Akizungumza Afisa Elimu Manispaa ya Songea Mwl. Janeth Moyo  kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea alisema Chama cha  Wauguzi Tanzania Tawi la Manispaa ya Songea kinaendelea na jitihada za makusudi za kukemea wauguzi wanaofanya kazi kinyume na makubaliano, kanuni na Sheria za kazi ya uuguzi, wauguzi kwani sio wauguzi wote ambao si waadilifu kwa wagonjwa n a jamii kwa ujumla. Alibainisha.

Aliongeza kuwa Serikali inaendelea na mikakati ya kuhakikisha inaweka mazingira mazuri ya kazi ya muuguzi pamoja na kuwawezesha wauguzi kuhudhuria mafunzo mbalimbali ya Taaluma na maadhimisho ya kimataifa ya siku ya Wauguzi pamoja na kuajiri watumishi wa ajira mpya.

Kwa upande wake Muuguzi Mkuu Manispaa ya Songea  Theodosia Ngowoko alisema Kauli Mbiu ya mwaka 2023 ni WAUGUZI MUSTAKABALI WA AFYA YETU” OUR NURSES OUR  FUTURE” Kauli mbiu hiyo inaangazia  umuhimu wa kuwalinda Wauguzi, kuwekeza katika fani ya uuguzi na kuheshimu haki za Wauguzi kwa kujenga mifumo thabiti ya Afya ya hali ya juu ili kukidhi mahitaji  ya  jamii.

Ngowoko aliongeza kuwa kuelekea kilele cha maadhimisho hayo shughuli mbalimbali za kijamii bila malipo zilifanyika ikiwemo na upimaji wa VVU, Huduma ya Uzazi wa Mpango, Uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa kizazi, Kutoa huduma ya Tohara, ambapo shughuli hizo zilianza kuadhimishwa kuanzia tarehe 10 Mei 2023 hadi siku ya kilele tarehe 12 Mei 2023. Alibainisha.

KAULI MBIU YA 2023;    WAUGUZI MUSTAKABALI WA AFYA YETU” OUR NURSES OUR  FUTURE”

Imeandaliwa na;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa