• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJILI UZINDUZI WA TAMASHA LA MAJIMAJI SEREBUKA MSIMU WA NANE.

Tarehe ya kuwekwa: July 25th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

25 JULAI 2022

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul (MB) ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuunga mkono Tamasha la Majimaji Serebuka ambalo linasaidia kukuza na kuendeleza sanaa na utamaduni nchini Tanzania.

Akizungumza katika uzinduzi wa Tamasha la Majimaji Serebuka msimu wa nane uliofanyika tarehe 23 Julai 2022 katika uwanja wa Majimaji Manispaa ya Songea, Mhe. Gekul alisema kuwa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo inaendelea na jitihada mbalimbali katika kuhakikisha inaendeleza pamoja na kulinda utamaduni nchini.

Aliongeza kuwa kwa mwaka fedha 2022/2023 Wizara imeweka vipaumbele mahususi kwa utekelezaji wa mfumo wa utamaduni na sanaa unaolenga kuwanufaisha wadau wa sekta ya sanaa nchini pamoja na kuanzisha  Tamasha la utamaduni la Kitaifa ambalo lilifanyika kwa mara ya kwanza Julai 1, 2022 jijini Dar es salaam.

Mhe. Gekul ametoa wito kwa viongozi wa Mikoa mingine nchini kuanzisha matamasha ya utamaduni katika Mikoa yao ili kuhakikisha yanaenea nchi nzima na kusaidia kukuza sanaa na utamaduni wa Taifa kwa ujumla.

Ametoa rai kwa viongozi wa Mkoa wa Ruvuma kutoa ushirikiano kwa kutoa maoni mbalimbali yatakayosaidia katika zoezi la uandaaji wa kitabu cha muongozo wa maadili ya Taifa la Tanzania ambacho kinalenga kupambana na mmong’onyoko wa maadili nchini kwa kuendeleza utamaduni wa Taifa kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Naye Muanzilishi wa Tamasha la Majimaji Serebuka Mhe. Damas Ndumbaro Waziri wa Katiba na Sheria (MB) alibainisha kuwa “Hili ni Tamasha la nane kufanyika tangu kuanza kwa Tamasha la Majimaji Serebuka ambapo litafanyika kwa muda wa siku nane”.

Ndumbaro ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kujitokeza kwa wingi kushuhudia muendelezo wa Tamasha hilo kwa siku zilizobaki ambapo hakuna kiingilio ni bure kabisa.”Alisisitiza”

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Pololet Kamando Mgema (Mkuu wa Wilaya Ya Songea) alisema kuwa tamasha la Majimaji Serebuka linasidia kuamsha Ari ya wanaruvuma kutambua, kuthamini na kuendeleza urithi wa utamaduni wa Mtanzania pamoja na kutoa fursa za ukuaji wa uchumi kwa wajasiriamali waliojitokeza kushiriki katika Tamassha hilo.’Alibainisha’

Pololet aliongeza kuwa Tamasha hilo linasidia kutangaza fursa za utalii na uwekezaji ziliopo ndani ya Mkoa wa Ruvuma pamoja na kuchochea mchango wa sekta ya Sanaa, utamaduni na Michezo katika maendeleo ya jamii.

Mwisho.

  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa