• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

YALIYOJIRI SIKU YA UZINDUZI WA KAMPENI YA UCHAGUZI MDOGO KATA YA MFARANYAKI

Tarehe ya kuwekwa: September 4th, 2023

Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Mjini  kikiongozwa na Mwinyi MSolomi ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya  Songea Mjini, tarehe 03 Septemba 2023  umefanyika uzinduzi wa Kampeni ya uchaguzi mdogo wa Udiwani kata ya Mfaranyaki kwa lengo la kutangaza  Mgombea wao ndugu  Christopher Kayombo ambaye anagombea  nafasi ya Udiwani katika  kata ya Mfaranyaki kupitia Chama Cha Mapinduzi.

Uchaguzi huo umekuja mara baada ya kutokea kwa  kifo cha aliyekuwa Diwani wa kata ya Mfaranyaki  Marehemu Ajira Kalinga ambaye alifariki  Dunia tarehe  06 Mei 2023 katika Hosptali ya  BOCHI  Jijini Dar es salaam  na kuzikwa katika  Makaburi ya Mfaranyaki  Mjini Songea.

Aidha, miongoni mwa vyama vya Siasa vilivyogombea katika nafasi hiyo ni Chama cha Mapinduzi “CCM”  UDP, ACT WAZALENDO, Chama cha Wananchi CUF, AAFP, pamoja NCCR MAGEUZI.


Akizungumza  wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Komredi Oddo Mwisho alisema  CCM imekuwa ikiendelea na utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi yenye ukurasa 303 ambapo kwa Manispaa ya Songea kupitia kata ya Mfaranyaki kuanzia mwaka 2020 imetekeleza miradi mingi ikiwemo na miundo mbinu ya Elimu kupitia ujenzi wa  madarasa kwa Shule za Msingi na Sekondari, Sekta ya Afya, Masoko,  pamoja na Ujenzi wa Barabara za mitaa  katika Kata ya Mfaranyaki ambao unatarajia kuanza hivi karibuni.

Aliongeza kuwa, Chama cha Mapinduzi ni chama pekee chenye kutetea haki za wananchi,  ambapo kutokana na ubora wa utendaji kazi imara  walipokea wanachama wawili 2 kutoka chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA  ambao walirudisha kadi za CHADEMA na kupokea kadi za CCM mbele ya wanachama wa CCM, na wananchi waliohudhuria mkutano huo ambao ulifanyika katika uwanja wa Stendi ya Lori kata ya Mfaranyaki.

 

Kwa upande wake Mgombea Christopher Fabian  Kayombo alitoa shukrani kwa  wanachama wa CCM kwa kumpitisha na kumpa ridhaa ya kugombea katika nafasi ya Diwani kata ya Mfaranyaki, na kuahidi kuwatumikia wananchi wa kata hiyo  mara atakapochaguliwa kuwa Diwani wa kata ya Mfaranyaki,  hatimaye aliomba kura kwa Wananchi.

Hata hivyo, mara baada ya mgombea kuomba kura kwa wananchi,  Komredi Oddo Mwisho alimkabidhi Ilani ya CCM kwa ajili ya ufuatiliaji na  utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika kata ya Mfaranyaki   iliyoanzishwa na ambayo haijaanzishwa utekelezaji wake kuanzia kipindi cha Uhai wa aliyekuwa Diwani  wa  kata hiyo hadi hivi sasa ili aweze kusimamia na kutatua changamoto za kata hiyo.

Uchaguzi mdogo wa Diwani unatarajia kufanyika tarehe 19 Septemba 2023.

IMEANDALIWA NA;                                                                               

AMINA  PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.  







Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa