MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameagiza hadi kufikia Septemba 30 mwaka huu vikundi vyote ambavyo bado havijalipa mikopo Yao waliochukua kupitia Benki za CRDB na TPB tawi la Songea wachukuliwe hatua za kisheria.Akizungumza kwenye kikao cha ufuatuliaji wa madeni kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea,Mndeme amesema Baraza la Taifa la Uwezesheji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Linadai vikundi,vyama vya ushirika na SACCOS zaidi ya shilingi milioni 197 ambazo walikopeshwa kupitia CRDB na TBP mkoa wa Ruvuma
VIDEO hii ni kwa ajili ya Mafunzo ya Mfumo wa Epicor 10.2 Version 1, Kwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa - TANZANIA.Jumla ya Halmashauri zote 185 nchini zinatumia mfumo wa EPICORTumia Link hii http://172.16.18.194 kwa Mawasiliano na Dawati la Msaada TAMISEMI.H
MKUTANO wa Kimataifa wa wanafunzi wanasayansi vijana wa Tanzania (YST) yamefanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Juliusi Nyerere jijini Dar es salaam.Tanzania mwaka huu umeshiriki katika maonesho ya nane ya Young Sciencist Tanzania ambapo takribani wanafunzi wa shule za sekondari zaidi ya 100 kutoka mikoa yote nchini wameshiriki.
Manispaa ya Songea imetoa wanafunzi walioshiriki katika maonesho hayo ambapo washindi hupata zawadi mbalimbali ambapo washindi wa mwaka 2017 walikwenda kushiriki katika maonesho ya wanasayansi vijana nchini Afrika ya Kusini katika mji wa Durban ambako walishinda katika kundi la teknolojia.Washindi hao pia walipata fursa ya kwenda kutembelea kiwanda cha simu nchini Swedeni.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa