AWAMU ya pili ya mgawo wa pikipiki 10 kati ya 21 zilizotolewa kwa Waratibu Elimu 21 wa kata 21 zilizopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma zimekabidhiwa leo katika viwanja vya ofisi ya Manispaa ya Songea.Waratibu Elimu Kata 11 tayari walikabidhiwa pikipiki 11 katika awamu ya kwanza.Pikipiki hizo zimetolewa kwa waratibu elimu kata 2894 katika nchi nzima lengo likiwa ni kuzitumia kusimamia maendeleo ya elimu katika kata zao.
HALMASHAURI ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma imefanikiwa kupunguza vyumba vya madarasa ya nyasi hali ambayo imepunguza utoro wa wanafunzi na kusaidia kuinua kiwango cha elimu.Zaidi fuatilia simulizi hii ya mabadiliko inayoweza kuleta mabadiliko katika Halmashuri nyingine nchini Tanzania
Spika wa Bunge Job Ndugai amepiga marufuku kwa Wabunge wote kutoingia Bungeni wakiwa na kope bandia na kucha Bandia, lakini pia amesema anaendelea kukusanya maoni kuhusu wale wanaojichubua ngozi zao ili nalo alifanyie maamuzi.Spika Ndugai amesema hayo kutolewa hoja ya madhara yatokanayo na kucha pamoja na kope bandia iliyotolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa