MTAZAME Mkurugenzi wa Kampuni ya TOPONE ya Songea Pascal Msigwa akielezea sababu za kuanzisha chuo cha ufamasia katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma
Mratibu wa Mafunzo ya Chuo hicho David Anderson amesema chuo hicho kinafaa vyote muhimu ambavyo vitatumika kwa wanachuo ikiwemo maabara yenye vifaa vya kutosheleza,maktaba,vyumba vya madarasa na mabweni.Hata hivyo amesema kwa kuanzia chuo hicho kinatarajia kuchukua wanachuo wasiozidi 200 na amezitaja sifa za kujiunga na chuo hicho ni wanafunzi waliomaliza kidato cha nne waliofaulu katika kiwango cha chini ni ufaulu wa D nne kati ya hizo D mbili katika masomo ya Sayansi Biolojia na Kemia na D nyingine mbili katika masomo mengine isipokuwa masomo ya Dini na Biashara.
Mkurugenzi wa Kampuni ya TOPONE LIMITED ambao ndiyo wamiliki wa Chuo hicho Pascal Msigwa amesema chuo hicho kinatarajia kufunguliwa Oktoba mwaka huu ambacho kwa kuanzia kitakuwa kinatoa mafunzo ngazi ya cheti ambayo yanachukua miaka miwili.Msigwa amesema chuo hicho kimesajiriwa na Baraza la Ufundi la Taifa (NACTE) na kupewa namba ya usajiri 184 na kwamba lengo la kuanzisha chuo hicho kuiunga mkono serikali ya Awamu ya tano ya kuzalisha watalaamu wa ufamasia hapa nchini ili kukabiliana na upungufu uliopo.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa