Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Juni 28, 2017 alikutana na timu ya wataalamu wa masuala ya umeme na ujenzi wa mabwawa ya maji ya kuzalisha umeme iliyotumwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn. kwa lengo la kubadilishana uzoefu na Tanzania.
Mtazame Rais Magufuli akizungumzia utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge Power Project).Mradi huo wa umeme utakapokamilika utaongeza megawati 2,100, zaidi ya megawati 560 zinazozalishwa katika miradi mingine ya maji.
Ujenzi wa awamu ya kwanza wa reli ya kisasa(SGR) umefikia asilimia 16,ukitarajiwa kukamilika Novemba mwaka huu.Reli hiyo itatumiwa na Reli yenye kasi ya kilometa 160 kwa saa na uendeshaji wake utakuwa wa umeme na mafuta
HIFADHI ya Taifa ya wanayama pori ya Serengeti nchini Tanzania imeibuka ya kwanza Afrika baada ya utafiti uliofanywa na kampuni ya utalii ya Safari Bookings, utafiti uliofanyika mtandaoni kupitia tovuti yake.
Hifadhi hiyo imepata alama 4.9 kati ya 5. Mwaka 2015 Serengeti ilishinda na kuwa hifadhi bora zaidi.Moja ya sababu za hifadhi hiyo kuwa bora zaidi ni uwepo wa wanyama wengi wakiwemo aina tano kubwa (Big Five) ambao ni Tembo, Simba, Faru, Chui na Nyati.Sababu nyingine ni kuwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni limetaja eneo hilo kuwa urithi wa dunia.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa