MNAZIBAY Ruvuma Marine Park ni kivutio muhimu cha utalii ambacho kinaonesha chanzo cha mto Ruvuma ambao umeanzia milima ya Matogoro Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ambacho kimeendelea hadi Mnazibay Marine PARK mkoani Mtwara kwenye maingilia ya mto Ruvuma katika Bahari ya Hindi.Mto Ruvuma ndiyo mto mrefu zaidi Afrika Mashariki na Kati.
Mtazame Afisa Maliasili na utalii wa Mkoa wa Ruvuma Africanus Challe anazungumzia vivutio vya kipekee na adimu ambavyo havipatikani sehemu nyingine yoyote Duniani zaidi ya hifadhi ya Gesimasoa iliyopo wilayani Songea mkoani Ruvuma . Hapa anazungumzia chanzo cha Mto Ruhuhu ambao upo kwenye hifadhi ya Gesimasoa ambapo kuna maingiliano ya mito Hanga na Lutukira inaunda mto Ruhuhu unaomwaga maji yake ziwa Nyasa.
MTAZAME Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Tina Sekambo akizungumzia maendeleo ya miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo inatekelezwa katika Manispaa ya Songea ikiwemo inayofadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo ni ujenzi wa barabara za lami,ujenzi wa machinjio ya kisasa,ujenzi wa stendi ya mabasi ya kisasa na ujenzi wa bustani ya manispaa ya Songea.Pia Manispaa inatekeleza miradi mingine mingi ya maendeleo.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa