TANZANIA ni miongoni mwa nchi chache duniani ambayo ina fursa za kipekee ambazo zinaweza kuchochea utalii wa ikolojia kupitia ziwa Tanganyika na ziwa Nyasa.
Maziwa hayo mawili yanatajwa kuwa na aina mbalimbali za samaki wa mapambo ambao baadhi yao wana sifa ya kutoa umeme hivyo wamepewa jina la samaki umeme(electric fish).
Utafiti wa awali ambao ulifanywa katika ziwa Tanganyika na Mwanasayansi Erick Fortune kutoka Chuo Kikuu cha Johns Hopkins cha nchini Marekani unaonesha kuwa samaki-umeme wana uwezo wa kutoa umeme kwa kutumia ogani umeme iliyopo kwenye mikia ya samaki hao.
MTAZAME Mchumi Mkuu wa Manispaa ya Songea Raphael Kimary wakati anatoa tahadhari kwa madiwani wa Manispaa ya Songea.Alikuwa anatoa mada ya namna serikali za mitaa zinavyochangia kusaidia kuendeleza miradi ya maendeleo
UDANGANYIFU ni tendo lolote la uamuzi au uasi unaofanywa kwa lengo la kuwadanganya wengine na kusababisha anayedanganywa kupata hasara na anayedanganya kufaidika ama kwa kupata fedha.Akitoa mada ya vihatarishi vya udanganyifu kwa madiwani,wataalam na maafisa watendaji wa mitaa na Kata wa Manispaa ya Songea katika mafunzo ya siku mbili,Mkaguzi wa Ndani wa Manispaa hiyo Joel Mantakara anasema tendo la udanganyifu hujumuisha wizi,rushwa na njama.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa