TAZAMA mabadiliko madogo ambayo yamefanywa na Rais Dkt.John Magufuli katika Baraza la Mawaziri na kufanya uteuzi wa makatibu wakuu na Naibu makatibu wakuu
SERIKALI za Mitaa katika Halmashauri za Wilaya,Miji,Manispaa na Majiji zimekuwa zinatambua,chambua na kuamua njia halisi na sahihi za kusaidia jitihada za jamii katika ngazi ya vitongoji,vijiji,mitaa na kata.
Mchumi Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma,Raphael Kimary anazitaja njia kuu ya kutumia njia shirikishi ni kutokana na ruzuku au fedha ya kutegemea serikali ni kidogo.Alikuwa akizungumza kwenye mafunzo ya jitihada za jamii katika kuchangia miradi ya maendeleo ambayo yametolewa kwa madiwani wa Halmashauri hiyo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.
MTAZAME Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea ambaye pia ni Diwani wa Kata ya subira Abdul Hasan Mshaweji anasema nia ya Halmashauri ni kusaidia jitihada za wananchi kwa kuwapa moyo na kuendeleza uwezo wa jamii hivyo ameshauri wadau wengine kushirikishwa ili kuchangia badala ya kusubiri serikali ambayo haina fedha za kutosha kutekeleza miradi.Alitoa maoni mara baada ya kupata mafunzo ya jitihada za jamii katika kuchangia miradi ya maendeleo yaliyoshirikisha madiwani wote wa Manispaa ya Songea Juni 29,2018.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa