Katibu Tawala mkoani Ruvuma Profesa Riziki shemdoe ambaye amewakilishwa na Katibu Tawala Msaidizi Edimund Siame, amefungua Mafunzo ya kuibua na kubadilishana simulizi za mabadiliko kwa maafisa Habari,Elimu na wenyeviti wa waratibu kutoka Halmashauri zote nane za mkoa wa Ruvuma.Mafunzo ya siku mbili ambayo pia yamewashirikisha wanahabari toka vyombo mbalimbali vya habari yanafanyika kwenye ukumbi wa kanisa katoliki Jimbo la Mbinga.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma pololet Mgema amesema NFRA Kanda ya songea imepata mgawo wa fedha toka serikalini wa kununua mahindi tani 6000
Shirika la Maendeleo la Taifa NDC limetoa semina elekezi ya upatikanaji wa matrekta kwa gharama na masharti nafuu kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.Semina hiyo imeratibiwa na Mbunge wa Viti Maalum Ruvuma.
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa