• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAMIA wajitokeza kupima homa ya Ini

Tarehe ya kuwekwa: July 28th, 2019

Na John Stephen

Wataalam wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wameadhimisha siku ya Homa ya Ini duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya kwa watu 375, huku 29  kati yao wakiwa wameambukizwa ugonjwa wa Homa ya Ini na 55 wakiwa wamepatiwa chanjo.

MNH imetoa huduma ya kupima watu mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Homa ya Ini duniani ambayo hufanyika tarehe 28 Julai kila mwaka.

Kati ya watu 375 waliojitokeza wanaume ni 175 na wanawake ni 200 ambapo watu 346 hawana ugonjwa wa Homa ya Ini.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini wa Muhimbili, Dkt. Masolwa Ng’wanasayi amesema watu waliobainika kuwa na Homa ya Ini wameshauriwa kwenda hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Dkt. Ng’wanasayi amesema lengo la kufanya uchunguzi wa afya kwa watu  mbalimbali ni kuongeza uelewa katika jamii kuhusu ugonjwa wa Homa ya Ini wa aina ya Hepatitis B.

Mtaalamu amebainisha kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO),  watu 325 milioni duniani wanaishi na maambukizi ya Homa ya Ini na kwamba asilimia nane ya wakazi wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara wameambukizwa Homa ya Ini aina ya Hepatitis B.

“Hapa kwetu tafiti zinaonyesha asilimia 4.9 wameambukizwa ugonjwa wa Homa ya Ini aina ya Hepatitis B na asilimia 2 wameambukizwa Homa ya Ini aina ya Hepatitis C,” amesema Dkt. Ng’wanasayi.

Amesema kundi la watu wanaotumia dawa za kulevya  ni miongoni mwa watu ambao wameambukizwa Homa ya Ini. “Tafiti zinaonyesha kwamba miongoni mwao asilimia 67 hadi 70 wameambukizwa Homa ya Ini,” amesema.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa