• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAFUNZI Songea kuanza kufundishwa kijiditali,DONBOSKO yatoa vishikwambi ,kompyuta na projekta

Tarehe ya kuwekwa: February 15th, 2019

SHIRIKA  la Kanisa katoliki la DONBOSKO Network limetoa vishikwambi 1824 ,kompyuta mpakato 38 na powepoint 19 katika shule kumi za msingi katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Mhasibu wa DONBOSKO padre Celestine Kharkongor  amesema vifaa hivyo vina thamani ya shilingi milioni 885 na kwamba lengo ni kuhakikisha walimu na wanafunzi wanatumia vifaa vya kieletroniki katika tendo la kujifunza na kufundisha na kuleta mapinduzi katika elimu.

Padre Celestine amesema mradi huu unafanyika katika awamu ya pili upande wa Zanzibar na wilaya  Songea mkoani Ruvuma,mradi unatekelezwa katika Halmashauri za Manispaa ya Songea na Halmashauri ya wilaya ya Songea.

 Amesema DONBOSKO imetoa masanduku 35 yenye vishikwambi 96 kwa kilashule,power point na kompyuta mpakato katika shule za msingi zilizopo kwenye mradi,vifaa vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.575.

Hata hivyo amesema awamu ya kwanza ya mradi huo ilianza mwaka 2017 katika shule za msingi katika mikoa ya Dodoma,Iringa,Dar es salaam,Kilimanjaro na Morogoro.

 Kwa upande wake Padre Peter Mutechura ambaye ni Mkurugenzi wa Shirika la DONBOSKO Network Tanzania  anayeshughulikia Maendeleo na elimu amesema kupitia  program hii  mwalimu atatumia vifaa vya kijiditali kama jukwaa la kufundishia na kuifanya wilaya ya Songea kuingia katika mfumo wa kisasa wa kufundishia.

Afisa Elimu Msingi katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Zakia Fandy amelishukuru shirika la DONBOSKO kwa kuanzisha mradi huo katika shule kumi za Manispaa ya Songea ambapo amesema hiyo ni fursa nyingine katika manispaa ya Songea.Hata hivyo amewaagiza walimu wakuu kuhakikisha mradi unatekelezwa kulingana na malengo yaliyowekwa na vifaa hivyo visitumike katika matumizi yasiyostahili.

Nelson Mahenge ni Mratibu wa DONBOSKO Network ambaye ni Mtalaam wa teknolojia ya habari hapa anazungumza program ya kutumia kompyuta,vishikwambi na power point itakavyokuwa inatumika kufundishia ambapo amesema vifaa hivyo vikichajiwa vinaweza kutumika kwa saa zaidi ya nane na kwamba mwalimu anaweza kufundisha hata kama umeme umekatika.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Februari 15,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa