• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WILAYA ya Nyasa inavyotekeleza mradi wa panda miti kibiashara

Tarehe ya kuwekwa: January 10th, 2019

Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma imeridhia kuongeza eneo la upandaji miti ya kibiashara kutoka hekari 3905 hadi 20000 ishirini elfu katika Kata ya Mpepo na Liparamba ili kupunguza uteemezi wa misitu ya asili na kuongeza chanzo cha mapato ya serikali.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Dougras Ruambo wakati akiwasilisha taarifa ya upandaji miti ya kibiashara aliyoitoa wakati wa kikao cha kamati ya ushauri cha Wilaya ya Nyasa kilichofanyika hivi karibuni katika Ukumbi wa Kepteni John Komba Mbamba-bay Wilayani Nyasa.

Alifafanua kuwa katika Wilaya ya Nyasa kuna miradi miwili ya upandaji miti na miradi hiyo ni wa shamba la Mpepo unaosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) na mradi wa upandaji miti wa watu binafsi unaofadhiliwa na Serikali ya Finland kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia mradi wa panda miti kibiashara na lengo la mradi huu ni kutekeleza sera ya misitu ya mwaka 1998 lenye dhumuni la usimamizi wa misitu na upatikanaji endelevu wa mazao na huduma za misitu.

Mkurugenzi Ruambo aliongeza kuwa shamba la miti la Mpepo lina ukubwa wa hekta 3905, katika kuboresha usimamizi shamba limegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni mapera (ipo katika kijiji cha Mtetema) likiwa na ukubwa wa hekta (815) sehemu ya kizota (ipo katika vijiji vya kihulunga, Mtetema na Lunyele) yenye ukubwa wa hekta 2728 na sehemu ya Ndondo ina ukubwa wa hekari 362.

Aliongeza kuwa ili kutimiza ufanisi wa madhumuni ya uanzishwaji shamba na uwekezaji wa Serikali wenye tija, lengo ni kufikia ukubwa wa hekari 20,000 hivyo juhudi kubwa ya pamoja inahitajika ili kufikia malengo haya.

Aidha kwa mwaka wa fedha 2017/2018 serikali kupitia TFS ilitenga fedha na kupanda miti na mpaka sasa jumla ya miti 222,200 sawa na hekta 200, aliitaja miti iliyopandwa ni aina ya misindano, pinusna, pinus, telcunumanii, patula miti hii imepandwa katika kijiji cha sehemu ya mapera iliyopo kijiji cha Mtetema.

Hata hivyo katika mpango kazi wa shamba wa mwaka 2018/2019 TFS imepanga kupanda hekta 300 za miti aina ya misindano (pines). Hekta hizi zipo kijiji cha Mtetema (200) na kijiji cha Mpepo (100) ili kufanikisha mpango huu tayari eneo hili limeandaliwa na hatua ya upandaji zimeanza hivyo upandaji huu utakamilika katika msimu huu wa mvua na hivyo jumla ya hekta 500 za miti ya pine zitakuwa zimepandwa.

Wakala wa huduma za misitu Tanzania kupitia shamba la miti Mpepo umekuwa mstari wa mbele katika kuchangia huduma za jamii katika maeneo yanayozunguka shamba la miti Mpepo. Aliyataja mafanikio hayo kwa ni umeboresha Miundombinu ya barabara na umetoa mabomba rola 17 na bati 60 kwa ajili ya kijiji cha Mtetema na umetoa saruji mifuko 60 kwa ajili ya kijiji cha Kihulunga.

Aliitaja michango mingine ni viriba kilo 40 mbegu za miti kilo 42 aina ya misindano na mikaratusi kwa ajili ya vijiji vya Lunyere, Kihurunga, Mtetema na Mpepo na Wilaya ya Mbinga. Utaalamu wa kuitunza miti hiyo unaendelea na wananchi wanaoishi kuzunguka eneo la upandaji miti wananufaika na ajira

Imeandaliwa na Netho Credo

Afisa Habari Wilaya ya Nyasa

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa