• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

AFISA ELIMU SEKONDARI MANISPAA YA SONGEA, AZIPONGEZA SEKONDARI ZA KATA KWA UFAULU WA MITIHANI KIDATO CHA NNE, KUPATA DARAJA LA KWANZA.

Tarehe ya kuwekwa: February 1st, 2021

Ni wajibu wetu kutambua juhudi za  walimu wetu ikiwa pamoja na  kupata haki zao za msingi,   “ kwahiyo walichokifanya ni wajibu wao.” Hongereni  walimu wa Manispaa ya Songea.

Pongezi hizo zimetolewa na Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Songea Devotha Luwungo katika ziara ya kutembelea shule ya Mateka Sekondari na Ruvuma Sekondari iliyofanyika  leo        01.02. 2021.

Devotha akitoa pongezi hizo  kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea alisema “mwaka 2020 kama  Halmshauri imejitahidi kwasababu haijarudi nyuma kutokana na baadhi ya shule mbili zimepanda ikiwemo shule ya Sekondari Mateka  na Ruvuma Sekondari ambapo  wanafaunzi wawili wamefanya vizuri zaidi  kwa kupata alama ya  ufaulu wa daraja la kwanza  1.7  (division 1.7).”  Hongereni walimu.

Akiwataja wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne 2020 ambao ulifanyika tarehe  23 novemba 2020,   Jackson Kasimu Matembo mwanafunzi wa Mateka Sekondari ambaye amepata daraja la kwanza (division 1.7) na Mwanafunzi Ayubu Mohamed Ayubu mwanafunzi wa Ruvuma Sekondari  ambaye amepata daraja la kwanza ( division 1.7).

Naye Mkuu wa shule Mateka Sekondari Melikizedeck Paul Makanja alisema Jackson ni mwanafunzi ambaye alikuwa anajitihada za kujisomea na alikuwa akiongoza darasa toka kidato cha kwanza hadi kidato cha nne  kwasababu katika matokeo yake ya kidato cha pili mwaka 2018 alifaulu na kupata daraja la 1.7, pia katika mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2020 mwanafunzi huyo amepata daraja la kwanza (division one) kwa ufaulu wa masomo alama A na B moja ya Kiswahili na C moja ya hesabu.

Makanja alisema Miongoni mwa mikakati ya shule waliyojiwekea kwa mwaka  2020 ilikuwa ni kuhakikisha wanaondoa  sifuri  0  ambapo kati ya wanafunzi waliosajiliwa mwaka 2020 walikuwa 66 kati ya hao waliofanya mtihani ni 63 ambao wote wamefaulu ambapo daraja la 1 wamefaulu wanafunzi 6, daraja la pili wamefaulu  wanafunzi 16, daraja 3 wamefaulu wanafunzi 14, na daraja la 4 wamefaulu wanafunzi 27 sawa na asilimia 100%.    Jackson Kasimu Matembo ni mtoto anayelelewa  na bibi yake kwani wazazi wake hawaishi pamoja (walitengana).

Naye Mkuu wa shule ya Sekondari Ruvuma  Altemius Altemius Komba alisema mwanafunzi Ayubu Mohamedi Ayubu ambaye amefaulu na kupata daraja la kwanza kwa kupata alama A - 7 na na alama B moja  na C moja. Katika mtihani wake wa kidato cha pili 2018 Ayubu Mohamed Ayubu alifaulu na kupata daraja la kwanza pointi 7 (division 1.7) hivyo matokeo hayo ni halali kuyapata kwani alikuwa akiongoza darasani kila muhula hadi kumaliza kwa masomo yake ya kidato cha nne 2020.

Komba aliongeza kuwa pamoja na matokeo mazuri ya mwananfunzi huyo lakini kuna wanafunzi wengine wawili ambao wamefanya vizuri kwa kupata daraja la kwanza ambao ni Kelvin Vitalis ambaye amepata      ( division 1.10) na  mwanafunzi Abdulazak Hamisi Alli ambaye amepata daraja ( division 1.11).

Aliongeza kuwa jumla ya wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani walikuwa 110, kati ya hao waliofanya mtihani ni 104 na matokeo yao ni daraja la 1 wamefaulu 8, daraja la pili wamefaulu 12, daraja la tatu wamefaulu 12, daraja la nne wamefaulu 58, na waliofeli ni 14. Mikakati waliyojiwekea ili kukabiliana na changamoto ya wanafunzi kufeli mtihani ni pamoja na kuhakikisha kila mwalimu anafundisha mada  kikamilifu.

Naye mwanafunzi Ayubu Mohamed Ayubu alisema anafuraha sana kupata matokeo mazuri kama hayo japokuwa alitarajia kupata  A katika masomo yake yote lakini hata hivyo  anamshukuru mungu kwa hatua aliyofikia. Alisema  yeye ni mtoto aliyekosa mzazi mmoja yaani baba ( alifariki 2011) na sasa anaishi na mama yake mzazi ambaye ni mjasiliamali mdogo wa  kuuza sweta.

Ndoto za wanafuzi hao kwa baadaye wamesema  ni kuwa madaktari.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

01 FEBRUARI 2021.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa