• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ASILIMIA 52 ya wenye VVU ndiyo wanajua hali zao

Tarehe ya kuwekwa: June 20th, 2018

UTAFITI wa nne uliofanyika katika ngazi ya kaya kuanzia Oktoba 2016 hadi Agosti 2017 ulibainisha kuwa wastani wa kitaifa wa maambukizi ya VVU kwa watu wenye umri wa miaka 15 hadi 49 ni asilimia 4.7. Wanawake ni asilimia 6.2 na wanaume ni asilimia 3.1.

Nchi yetu imeridhia na kuanza utekelezaji wa kauli mbiu ya kidunia ya ifikapo 2020 ya asilimia 90 ya watu wanaoishi na VVU wawe wamejua hali zao za maambukizo,asilimia 90 ya waliopimwa VVU na kugundulika kuwa wana maambukizo wapatiwe dawa za kufubaza makali ya VVU na asilimia 90 ya watu wanaotumia dawa wawe wamefubaza VVU.

 Nchini Tanzania ni asilimia 52.2 tu ya wanaoishi na VVU wenye umri wa miaka 15 – 64 ndiyo walitoa taarifa kuwa wanaojua hali zao za maambukizo ya VVU  ambapo Wanawake ni asilimia 55.9 na Wanaume ni asilimia 45.3

Kati ya watu wanaoishi na VVU wenye umri wa miaka 15 – 64 ambao wanajua hali zao za maambukizo ni asilimia 90.9 ndiyo  walitoa taarifa kuwa wanatumia dawa za kufubaza VVU kati yao Wanawake ni asilimia 92.9 na Wanaume ni asilimia 86.1.

Kati ya watu wanaoishi na VVU wenye umri wa miaka 15 – 64 ambao wametoa taarifa kuwa wanatumia dawa za kufubaza VVU,asilimia 87.7 ya watu hao inaonesha kiasi cha VVU kimefubazwa,kati yao Wanawake ni asilimia 89.2 na Wanaume ni asilimia 84.

Hivyo basi, Kulingana na utafiti huo Tanzania inafanya vizuri,hata hivyo lakini tatizo kubwa ni katika kufikia 90 ya kwanza, kwa kuwa ni asilimia 52.2 tu ya wenye VVU wanajua hali zao. Tatizo hili ni kubwa zaidi miongoni mwa wanaume, kwa sababu ni asilimia 45.3 tu ya wanaume wanaoishi na VVU wanajua hali zao.

Madhumini ya kampeni hii ni kufikia malengo ya Tanzania kwamba ifikapo mwaka 2020 asilimia 90 ya watu wanaoishi na VVU wawe wanatambua hali zao za maambukizi, asilimia 90 kati yao wanatumia ARV na asilimia 90 ya wanaotumia ARV kiwango chao cha VVU mwilini kinashuka.


Malengo ya kampeni ni kusaidia kutimiza malengo ya Tisini tatu (90 90 90) kwa kuzingatia malengo yaliyowekwa Kitaifa na Mikoa.

Mikoa ya utekelezaji wa mradi wa Tulonge Afya (Upande wa Uhamasishaji) na Boresha Afya (Upande wa Utoaji wa Huduma) ni Arusha, Kagera, Geita, Shinyanga, Kigoma,Mara,Mwanza,Tabora, Singida, Iringa, Njombe, Mtwara, Morogoro, Lindi, Ruvuma, Dodoma Kilimanjaro, Manyara na Simiyu.

Walengwa wa kampeni hii ni Watu ambao hawajawahi kupima VVU na wako katika hatari ya kumbukizwa au kuambukiza VVU:

Wanaume wenye Umri chini ya Miaka 45,Wasichana walio katika umri wa balehe,Wanawake wenye umri wa miaka 15-24,Akinamama wajawazito,Watu ambao wameambukizwa VVU na hawajaanza kutumia ARV na Akina Mama wanaoishi na VVU na Wananyonyesha na watoto wao.

Njia za Mawasiliano ambazo zinatumika kukabiliana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI ni ,Radio za Kitaifa,Radio za mikoa au kijamii,mitandao ya kijamii,televisheni,watoa huduma za Afya na walielimisharika,mawasiliano ya ana kwa ana,Machapisho ya aina mbalimbali na Mikutano ya ulaghabishi kitaifa,mikoa na wilaya.

Makala imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari serikalini

Juni 20,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa