• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ASILIMIA zaidi ya 60 ya Tanzania ni jangwa

Tarehe ya kuwekwa: June 17th, 2018

TATIZO la  ukataji wa miti na misitu hovyo limesababisha nchi yetu  kuwa na zaidi ya asilimia 60 ya eneo lililoathiriwa na jangwa kwa kuwa vyanzo vingi vya maji vimeendelea kukauka mwaka hadi mwaka.Takwimu zinaonesha kuwa nchi yetu kila baada ya wastani wa miaka minne kunatokea ukame na kuathiri karibu watu milioni 3.6 katika Sehemu za Dodoma, Singida, Shinyanga, Mwanza na Mara.

kutokana na ukataji wa misitu, kilimo kisicho cha kitaalam kumesababisha mmomonyoko wa ardhi na kusababisha udongo kupoteza rutuba na hivyo kusababisha ukosefu wa mvua na mafuriko ambayo  huwaathiri wananchi kila mwaka.Uharibifu wa mazingira nchini sio unaleta athari katika ardhi na maji tu lakini pia unachafua hewa na kusababisha madhara makubwa kwa afya ya wanadamu na viumbe vingine hai ambavyo hutegemea hewa safi ili viweze kuendelea kuishi.

Hali halisi inayoendelea hivi sasa inathibitisha kuwa taasisi zinazoshughulikia mazingira zimeshindwa kuzuia uharibifu wa mazingira licha ya kuwepo sera na sheria matokeo yake watanzania wengi wanapata athari za kiafya na kimazingira hali hii ni mbaya kwa kuwa siku moja tunaweza kuangamia sote.

Kutokana na uchafuzi huo wa mazingira historia inaonesha kutoka mwaka 1980 hadi 2015 mafuriko nchini mwetu yameshatokea mara nyingi na kusababisha vifo vya watu  na wengine kuathiriwa vibaya katika makazi yao hasa katika Sehemu za Tanga,Dar es salaam, Mbeya, Zanzibar, pemba,Geita,Shinyanga, Pwani, Morogoro, Arusha, Rukwa, Iringa, Kigoma,Lindi na Dodoma.

 Sheria zipo kinachotakiwa ni kuhakikisha sheria hizo zinachukua nafasi yake kwa wale wote watakaobainika kwenda kinyume na sheria za mazingira ukiwemo ukataji wa misitu na uchafuzi wa vyanzo vya maji.Tusipoangalia vita kuu ya tatu ya Dunia ambayo itasababishwa na uchafuzi na uharibifu wa mazingira inakuja ambayo italeta maangamizi makubwa kwa viumbehai wakiwa binadamu.

Mwandishi wa makala haya ni Albano Midelo.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa