• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA NA KUIDHINISHA RASIMU YA BAJETI 2025/2026

Tarehe ya kuwekwa: February 13th, 2025

Baraza la Madiwani Manispaa ya Songea limepitisha bajeti ya shilingi 55,686,483.00  kutoka kwenye vyanzo mbalimbali katika kipindi cha mwaka  wa fedha 2025/2026.

Baraza hilo limefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea tarehe 12 februari 2025 ambalo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali ngazi ya Chama, Waheshimiwa madiwani pamoja na wakuu wa idara na vitengo na wadau mbalimbali kwa lengo la kupitisha rasimu ya mpango na bajeti ya mwaka 2025/2026.

Akisoma taarifa hiyo kwenye baraza la Madiwani Mchumi wa Manispaa ya Songea Wilfredy Razaro alisema, vyanzo vya mapato ni kiasi cha sh. 8,318,668,000.000, mishahara ni shilingi 36,990,880,000.00, matumizi mengine kutoka Serikali kuu shilingi 1,874,749,000.000 ambapo ruzuku ya miradi mbalimbali ya maendeleo ni 3,563,995,000.00 na vyanzo vya ndani Halmashauri hiyo ni 4,938,619,483,000.

Razaro alibainisha vipaumbele katika Halmashauri hiyo ni  kutoa nafasi kwa watumishi kujiendeleza kupitia semina, mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwenye vyuo mbalimbali pamoja na semina na mikutano ya kitaaluma, kutenga madeni ya watumishi  na zabuni, upatikanaji wa vitendea kazi, stahiki mbalimbali za watumishi, Mazishi, likizo pamoja na matibabu. “Alieleza”  

Aliongeza kuwa vipaumbele vingine ni ununuzi wa gari kwaajili ya kurahisisha utendaji wa kazi  wa watumishi katika kusimamia majukumu  pamoja na mahitaji maalum kutokana na wagonjwa kwa ustawi wao kazini.

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano kwa kushirikiana na Madiwani hao  mara baada ya kuridhia na kupitisha rasimu ya mpango na bajeti 2025/2026  amewataka madiwani hao kuendelea kutoa ushirikiano katika kusimamia miradi ya maendeleo inapoelekea kipindi cha uchaguzi huku akiwataka kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.

Akitoa pongezi kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi za kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo maji, elimu, barabara na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Kwa upande wakeMbunge wa jimbo la Songea Mjini Dkt. Damas Ndumbaro (MB) Waziri wa Katiba na Sheria amewataka madiwani kujipongeza kwasababu ya kuteuliwa kwa Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea mwenza wa nafasi ya makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa ambapo kupitia mkutano mkuu wa CCM Taifa ulimpendekeza Dkt. Samia Suluhu Hassani kuwa mgombea wa Urais na Dkt. Hussein Mwinyi kuwa mgombea Urais Zanzibar.

Dkt. Ndumbaro alisema kila kata kuna miradi ambayo imetekelezwa hivyoMadiwani mna haki ya kujivunia kutokana na utendaji wa kazi zilizofanyika.

MWISHO:                                                                     

NA  AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.








Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Apongeza kwa Utekelezaji wa Miradi

    May 05, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Awataka Waajiri kuzingatia Misingi ya Utawala Bora

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Songea Akizindua Stendi ya Bajaji - Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa