• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SONGEA KUIDHINISHA MPANGO NA BAJETI 2021/2022.

Tarehe ya kuwekwa: March 2nd, 2021

Baraza la Madiwani Manispaa ya Songea limeidhinisha  makisio   ya bajeti ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kiasi cha Tsh 39,046,546,758.33 kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya Halmashauri.

Mstahiki Meya Halmashauri ya Manispaa ya Songea Michael Mbano ambaye  pia ni mwenyekiti wa baraza la Madiwani  alisema kwa kupitia baraza hili tumeidhinisha  mpango na bajeti ya maendeleo wa mwaka wa fedha 2021 hadi 2022,  hivyo ametoa rai kwa  madiwani hao kutoa ushirikiano kwa wataalamu  katika kusimamia miradi ya maendeleo iliyopo kwenye maeneo yao.

Baraza hilo limefanyika tarehe 01 machi 2021 na kuidhinishwa kukusanya na kutumia kiasi cha fedha 39,046,546,758.33 kwa ajili ya miradi  mabalimbali ikiwemo na miradi ya maendeleo.  Kati ya fedha hizo mapato ya ndani ni kiasi cha Tsh  cha shilingi 4,329,012,060.00 makisio ya mapato ya ndani ambayo ni Zaidi ya shilingi 354,757,770.00 sawa na asilimia 8.2 ukilinganisha na makisio ya mwaka 2020/2021 yalikuwa 3,974,254,060.00.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo alisema katika mpango na bajeti ya maendeleo wa mwaka wa fedha 2021/2022, Halmashauri ya Manispaa ya Songea inatarajia kukusanya na kutumia kiasi cha shilingi 6,793,556,522.33 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo na mapato halisi ya ndani, ruzuku ya Serikali kuu, na Wahisani.

Tina alisema kuwa fedha hizo  zitazokusanywa kutoka kwenye mapato  mbalimbali ndizo zinazokwenda kutekeleza miradi ya maendeleo.  Hata hivyo, Amewataka madaiwani hao kutoa ushirikano kwa wataalamu  wakati wa kutekelezaji wa zoezi la ukusanyaji wa mapato ili kuweza kufanikisha kutatua changamoto mbalimbali zinzoikabili Halmashauri hiyo.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya Hamisi Abdalah Ally akichangia hoja katika baraza hilo ambapo amewataka Madiwani hao kuitisha mikutano ya wananchi kwenye kata zao na kuwashirikisha wataalamu  kwaajili ya kusikiliza kero na malalamiko  na kuzitafutia ufumbuzi  haraka iwezekanavyo  badala ya kusubili viongozi wa ngazi ya juu kuja kutatua kero zao.

Hamisi aliongeza kuwa wananchi wana kero nyingi  na ninyi Madiwani  ndiyo wawakilishi kupitia maeneo yenu lakini hamuitishi mikutano. Endapo mtawashirikisha wataalamu kwenye mikutano hiyo mtaondoa kero zinazowakabili wananchi kwani wataalamu na Madiwani ni ndugu hufanya kazi kwa kutegemeana.

Naye Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro ambaye ni Waziri wa Maliasili na Utalii alisema kila Wilaya ilipangiwa  kuwepo kwa hospitali  ya Wilaya lakini baadhi ya Wilaya ina Halmashauri Zaidi ya moja, hivyo kutokana na changamoto hiyo Serikali imeweka mpango wa kujenga Hosptali kila Halmashauri lakini haizuwii kuweka mkakati wa ujenzi wa Hosptali ya Mkoa .

Dr. Ndumbaro (MB) alimpongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea  pamoja na Wataalamu wate walioshiriki kuandaa mpango na bajeti hiyo ambayo imezingatia vitu muhimu.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

02.03.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa