• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Baraza la Madiwani Manispaa ya Songea Kumthibitisha Naibu Meya.

Tarehe ya kuwekwa: August 27th, 2022

Na; 

Amina Pilly;

Afisa Habari.

Serikali za Mitaa ni vyombo vilivyoanzishwa kwa mujibu wa ibara ya 145 na 146 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ya mwaka 1977,  pamoja marekebisho yake ambayo majukumu na muundo wa Mamlaka za Serikali za Mitaaa yameainishwa katika Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) sura ya 287 na sheria ya Serikali za Mitaa za mamlaka ya Miji sura 288.

Lengo la Mwongozo huo ni kuwawezesha  Madiwani na Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuelewa taratibu muhimu za uitishaji na uendeshaji wa mikutano ya kwanza ya Halmashauri baada ya uchaguzi  Mkuu.

Hayo yamebainishwa leo 27 Agosti 2022 katika Mkutano wa Mwaka  wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea  uliohudhuriwa na wananchi, wataalamu, na viongozi wa vyama vya siasa uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kumthibitisha Naibu Meya na  kuunda kamati za kudumu pamoja na kupokea taarifa ya mwaka.


Mstahiki Meya Manispaa ya songea Michael Mbano ambaye pia ni  Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo amewataka Madiwani kuzingatia agenda  zilizopo katika kikao hicho ili kupanga mikakati endelevu kwa maendeleo ya Taifa.

Mhe. Mbano amewapongeza wataalamu kwa kufanikisha zoezi la kuwapanga wamachinga katika maeneo yaliyotengwa  rasmi kwa kufanyia biashara hizo. Sambamba na pongezi hizo  ametoa Rai kwa wataalamu hao kuendelea  kufanya kazi kwa weredi ikiwemo na kuwa na tabia ya kutembelea miradi  mbalimbali ili kuweza kutatua changamoto  au malalamiko ya wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt. Frederick  Sagamiko alisema  kwa mujibu wa miongozo na kanuni Naibu Meya atatangazwa kuwa amechaguliwa endapo atakuwa amepata zaidi ya nusu ½ ya kura zilizopigwa.

Dkt. Sagamiko aliongeza kuwa  iwapo wakati wa kumchagua Naibu Meya kutakuwa na jina moja tu ambalo litakuwa limependekezwa, wajumbe watapiga kura za siri za “ndiyo” endapo zitazidi asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwa basi mgombea atatangazwa kuwa Naibu Meya na iwapo kura za hapana zitazidi asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwa, jina la mgombea mwingine litapendekezwa kwa njia na utaratibu uliotumika hapo awali. 


Aidha baada ya kusoma mwogozo huo hatua za uchaguzi wa kumpigia kura mgombea Jeremia  Mlembe ambaye hakuwa na mpinzani uliendelea kufanyika na kwa kupigiwa kura na wajumbe ambao ni waheshimiwa madiwani  28 ambapo kura zilizopigwa ni 27, kura zilizoharibika 0, kura zilizokataliwa ni 0, na kura za ndiyo ni 27 ambapo baada ya matokeo hayo katibu wa Baraza la Madiwani Manispaa ya Songea kwa mamlaka aliyopewa alimtangaza Mhe. Jeremiah Mlembe Diwani wa Kata ya Bombambili kuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Songea.

Baada ya kukamilisha kusimamia zoezi la kumthibitisha Naibu Meya, aliziitambulisha kamati mbalimbali za kudumu za halmashauri ikiwemo na kamati ya fedha, kamati ya mipango miji, kamati ya uchumi na kamati ya maadili na kisha alisoma taarifa utekelezaji wa shughuli mbalimbali za mwaka mmoja 2021 hadi 2022.

Naye Naibu Meya Jeremiah Mlembe alitoa shukrani kwa wajumbe wote waliomchagua nakuahidi kutoa ushirikiano baina ya Waheshimiwa Madiwani na wataalam.

Mwisho.


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa