• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BENK YA NMB-SONGEA YATOA MSAADA WA MADAWATI KWA SHULE ZA MSINGI WENYE THAMANI YA MIL. 12.

Tarehe ya kuwekwa: March 12th, 2021

Benki ya NMB tawi la Songea imetoa msaada wa madawati, meza, kabati na bati kwa shule za Msingi tatu 3 za Manispaa ya Songea yenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 12.

Msaada huo umetolewa jana tarehe 11 machi 2021 kwa shule ya Msingi Legele ambapo walipata bati 60, Shule ya Msingi Mshangano kati walipata madawati 80 pamoja na shule ya Msingi Chandamali  walipata viti na meza na kabati kwa ajili ya matumizi ya ofisi za walimu.

Mgeni rasmi katika zoezi hilo la ugawaji wa vifaa vya shule ni mkuu wa Wilaya ya Songea ambaye aliwakilishwa na katibu Tawala Wilaya ya Songea Bi Pendo Daniel ambaye alianza kwa kutoa shukrani kwa Benki ya NMB kwa utamaduni  walionao wa  kutoa msaada kwa jamii mara kwa mara ambayo ni 1% ya faida wanayoipata kutoka kwa wateja wao.

Bi Pendo amewataka wadau wengine kuwa na desturi ya kusaidia jamii  kama wafanyavyo wadau wa Benki NMB  kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuchangia huduma bora za Afya, Elimu bure na za kijamii.

Ametoa Rai kwa jamii kuhamasika kwa wingi kufungua akaunti  Benki ya NMB ili waweze kutoa msaada zaidi kwa jamii.

Naye Meneja wa kanda wa Benk NMB Janeth Shango alisema lengo la NMB ni kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano ambayo inahakikisha inatoa huduma bora za afya, Elimu na huduma nyingine za kijamii.

Shango alisema NMB wanao wajibu wa kushirikiana na Serikali ili kuweza kutatua changamoto ambazo zinapatikana katika maeneo ya kijamii ambapo imejikita kusaidia katika sehemu ya Elimu ambapo huchangia baadhi ya mahitaji ikiwemo na madawati kwa shule za msingi, viti na meza kwa shule za sekondari pamoja na sekta ya Afya husaidia vitanda na magodoro pamoja na bati za kuezekea majengo mbalimbali.

Alisema NMB imekuwa na utamaduni wa kurudisha faida kwa jamii ambayo inaipata katika jamii ambayo inaizunguka kwa kutoa msaada ambao unatokana na 1% ya faida waipatayo kutoka kwa wateja wao kwa kutokana na desturi hiyo, Benki ya NMB mwaka 2020 imefanya vizuri katika soko kwa masuala ya kibenki na imetengeneza kiwango kipya cha upatikanaji wa faida nchini.

Aidha, kupitia huduma hizo Benki ya NMB imekuwa bora kwa miaka 8 nane mfululizo na ndani ya muda huo wamekuwa wakiendelea  kutoa 1% ya faida wanayoipata kuchangia shughuli mbalimbali za kijamii.

Naye afisa Elimu Msingi Manispaa ya Songea Zakia Fandey alitoa shukrani kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa na kisha alisema Halmashauri ina   jumla ya shule za msingi 92 kati ya hizo shule tatu 3 zimepokea msaada wa madawati, bati, kabati, viti na meza kutoka Benki ya NMB ambapo amewataka walimu wa shule hizo  kuhakikisha  wanatunza vizuri vizuri ili viweze kumudu kwa muda mrefu.

IMEANDALIWA NA;                                                                                                 

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

12.03.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa