• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BIL.1.52 KUJENGA MADARASA 76 MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: October 11th, 2022

Baraza la Madiwani Manispaa ya Songea likiongozwa na Mstahiki Meya Michael Mbano kwa kushirikiana na wataalamu  wametoa Pongezi za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Samia Suluhu Hassani kwa kutoa kiasi cha fedha Bilion 1.520,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 76 katika shule za Sekondari.

Pongezi hizo zimetolewa katika  Mkutano wa Baraza la Madiwani liliofanyika tarehe 10 Oktoba kwa ajili ya kutoa taarifa za mapokezi ya fedha Bil. 1.52, na kupokea mrejesho wa mpango na bajeti ya Halmashauri iliyoidhinishwa na Serikali ambayo itatekelezwa mwaka wa fedha 2022/2023, pamoja na kupitisha majina ya wajumbe wa bodi ya maji kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa  ya Songea na kuhudhuriwa na waheshimiwa madiwani, wataalamu na wananchi.

Mhe. Mbano akielezea kuhusu mpango kazi na mikakati iliyojiwekea Manispaaa ya Songea katika kufanikisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 76  ni pamoja na kushirikisha wananchi kuhusu mapokezi ya fedha za mradi kwa kufanya mikutano ya hadhara ifikapo tarehe 11/10/2022  kwa kata zote na mitaa, pamoja na kufuata muongozo wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Amewataka Madiwani na wataalamu  kutumia nafasi zao kuwaeleza wananchi shughuli mbalimbali na mafanikio yanayotekelezwa na Serikali ili wananchi waweze kufahamu miradi ya   maendeleo inayoendelea kufanyika katika Serikali yao.

Alisema miongoni mwa miradi inayoendelea kujengwa Manispaa ya Songea ni pamoja na  kituo cha afya Lilambo kwa fedha za mapato ya ndani pamoja na vituo vya afya  Mletele, kituo cha afya Subira, Kituo cha afya Msamala, Hospital ya Rufaa inyojengwa Mwenge mshindo, pamoja na Hpsptali ya Wilaya Songea kwa fedha kutoka Serikali kuu. “ Alibainisha”

Mh. Mbano amewaagiza maafisa watendaji wa kata na mitaa wote kuhakikisha wanaweka ulinzi shirikishi katika maeneo wanayoyaongoza ili kuzuwia matukio mbalimbali ya wizi wa ng’ombe ambayo yamekuwa tishio katika jamii na utekelezaji wa agizo hilo unatakiwa kuwasilishwa kwenye kikao kazi cha Madiwani ambacho kinatarajia kufanyika hivi karibuni. Alisisitiza

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Songea Andambike Kyomo  alisema Manispaa ya Songea imepokea fedha kutoka Serikali kuu  kiasi cha Bil.1.52 kwajili ya ujenzi wa  vyumba vya madarasa 76  ambayo yatajengwa katika mfumo wa FORCE ACCOUNT ambao unatakiwa kukamilika  ifikapo  tarehe 15 disemba ambapo utajumuisha utengenezaji wa samani ambazo ni viti 50 na meza 50.

.

Kyomo, akitoa maelekezo juu ya mrejesho na bajeti iliyoidhinishwa ambapo alibainisha kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea  kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imeidhinishwa kukusanya na kutumia kutoka kwenye vyanzo mbalimbali jumla ya shilingi 45,635,750,000 kati ya fedha hizo, fedha za mapato  ndani ni 5,517,867,000.00, shilingi 35,842,547,000.00 ni fedha za Serikali ambapo shilingi 4,275,336,000.00 ni fedha za wafadhili.

Akifafanua  kuhusu namna ya uundaji wa Bodi ya maji Manispaa ya Songea “ kwa Mujibu wa Sheria namba 5 ya Maji na Usafi wa Mazingira 2019 ambayo inasema  mchakato wa kuwapata wajumbe wa bodi ya maji ambao unapitia baraza la madiwani  watapendekeza  majina ya  wajumbe watakaounda  bodi mpya ya  maji  baada ya bodi iliyopita kumaliza muda wake na  majina hayo yapitishwe kwenye baraza la madiwani ili yaweze kupelekwa Wizarani kwa ajili ya kuteuliwa kupitia nafasi za mjumbe mwakilishi wa watumiaji wa maji,  mwakilishi wa wanawake, na mwakilishi wa madiwani. Mwisho wa kunukuu”


Mwanasheria kutoka SOWASA Abel Ngilangwa alisema kwa mujibu wa sheria na taratibu za kupata wajumbe wa bodi zinapitia katika mchakato wa kupata mjumbe mmoja  kutoka Wizara ya maji, Mjumbe kutoka Mkoa na Halmashauri, mjumbe kutoka baraza madiwani, mjumbe kutoka kwa watumiaji wa maji, na mjumbe mwakilishi wa wanawake.

Ngilangwa alibainisha kuwa bodi ya maji Safi na Mazingira na mamlaka nyingine zinaongozwa kwa mujibu wa sheria namba 5 ya mwaka 2019 na kanuni zake za mwaka 2019 ambazo zinafafanua sifa za watakaopendekezwa ni lazima awe mkazi husika, awe mlipaji mzuri wa maji na awe na elimu ya kidato cha sita au diploma.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Songea Mjini Mwinyi Msolomi amewataka madiwani  wote  kuandaa kikao cha tathimini ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa muda wa miaka mitano 5 ili kubaini changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.  

Msolomi ametoa Rai kwa Maafisa Watendaji kata wote na mitaa kuunda kamati za ulinzi na usalama kwenye maeneo yao ili kuzuwia matukio ya wizi hususani wizi wa ng’ombe ambao unaripotiwa mara kwa mara kutoka kwa wananchi.

 

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

MANISPAA YA SONGEA.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa