• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

CHUO cha CBCTC mkoani Ruvuma kuanza kutoa kozi ya waongoza watalii

Tarehe ya kuwekwa: June 6th, 2019

CHUO cha Mafunzo ya Uhifadhi wa Maliasili kwa Jamii (CBCTC) kilichopo katika Kijiji cha Likuyu Sekamaganga wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma  kimefanya mahafali ya mafunzo kwa Askari wanyamapori wa vijiji (VGS) ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Constantine Kanyasu.

Akizungumza katika mahafali hayo Naibu Waziri Kanyasu amewaasa askari wahitimu kwenda kuzilinda na kuzitunza rasilimali za taifa katika maeneo yao  ili ziwe endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Kanyasu ameahidi kushughulikia changamoto zinazokikabili chuo hicho ikiwemo miundombinu chakavu na kumalizia jengo la maktaba ambalo Naibu Waziri huyo ameweka jiwe  msingi na kwamba amesema serikali itahakikisha kuwa chuo hicho kinakuwa na sifa za chuo cha kati.

Awali akizungumza kabla ya mgeni rasmi Mkuu wa  chuo cha (CBCTC) Jane Nyau amesema chuo hicho  kilichoanzishwa mwaka 1995 ni Chuo pekee cha utoaji wa mafunzo ya uhifadhi wa maliasili kwa jamii barani Afrika na kwamba hapa nchini katika vyuo vya uhifadhi ,hakuna chuo kinachotoa mafunzo yanayofanana na chuo hiki,hali hiyo ndiyo inakifanya kuwa ni  chuo cha kipekee nchini.

Amesema katika mahafali ya kozi namba 64/2019  ya Askari wanyamapori wa vijiji(VGS)  jumla ya wanachuo 20 wamehitimu  mafunzo ya Askari wanyamapori wa vijiji (VGS) kwa miezi mitatu.

Nyau amesema licha ya chuo hicho kutoa kozi  za mafunzo ya Askari wanyamapori wa vijiji(VGS) ya miezi mitatu na mafunzo ya viongozi wa serikali na Kamati za maliasili za vijiji ya mwezi mmoja,CBCTC kuanzia Julai 2019 kinatarajia kuanza kutoa kozi ya Astashahada ya Awali ya Waongoza watalii kwa muda wa mwaka mmoja.

“Kozi hii  itatolewa ili kuendana na mkakati unaoendelea wa serikali wa kukuza utalii katika Ukanda wa Kusini,mtaala wa kozi hiyo umeshakamilika na tayari umeshathibitishwa na Baraza la Usimamizi wa Vyuo vya Ufundi (NACTE)’anasema Nyau.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Serikalini

Juni 5,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa