• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

CHUO cha mafunzo ya ulinzi Kunduchi wafanya ziara Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: January 7th, 2020

WAGENI wanaosoma katika chuo cha mafunzo ya ulinzi Kunduchi jijini Dar es salaam wamefanya ziara ya mafunzo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kujifunzo mambo mbalimbali katika Mkoa wa Ruvuma ikiwemo ulinzi na usalama .

Wageni hao ambao ni maafisa kutoka ndani na nje ya nchi wakiwa katika Manispaa ya Songea walikutana na mwenyeji wao Mwakilishi wa  Mkuu wa Wilaya ya Songea.Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassan Mshaweji na Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo.

Wakiwa katika ukumbi wa Manispaa  ya Songea,maafisa hao walipewa taarifa ya Manispaa ya Songea ikiwemo taarifa ya fedha ambayo inaonesha kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2019/2020  Manispaa imekuwa na bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 39,ambapo mapato ya ndani ni zaidi ya shilingi bilioni tatu.

Kulingana na taarifa hiyo,Manispaa ya Songea inatekeleza miradi mbalimbali katika Kata zote 21 zilizopo katika Manispaa  hiyo na kwamba Manispaa hiyo inatekeleza miradi mikubwa inayofadhiliwa na Benki ya Dunia ikiwemo ujenzi wa machinjiio ya kisasa uliogharimu zaidi ya shilingi bilioni 3.2 ,ujenzi wa kituo cha mabasi ya kisasa uliogharimu zaidi ya shilingi bilioni 6.1 na ukarabati wa barabara katika kiwango cha lami nzito zenye urefu wa kilometa 10.3 uliogharimu zaidi ya bilioni 10.

Maafisa hao katika Wilaya ya Songea wanatembelea Makumbusho ya Taifa ya Majimaji,Uwanja wa ndege wa Songea,Shamba la Kahawa la AVIV,kiwanda cha Sausage Peramiho,jengo la kihistoria la Kanisa katoliki la Peramiho na Wakala wa hifadhi ya chakula ya Taifa NFRA.

Kulingana na taarifa ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,maafisa hao wanatarajia kutembelea Mkoa wa Ruvuma katika Wilaya za Mbinga kwa kutembelea kiwanda cha kukoboa kahawa na wilaya ya Nyasa kwa kutembelea fukwe za ziwa Nyasa na kwamba ziara hiyo inatarajia kukamilika Januari 11,2020.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Serikalini

Januari 7,2020



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa