• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA, KUJENGA TAWI JIPYA MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: February 15th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

15.02.2022

Halmashauri ya Manispaa ya Songea yatoa eneo la hekari 71 kwa ajili ya ujenzi wa tawi la chuo kikuu cha uhasibu kilichopo Arusha  hapo jana Februari 14, 2022 katika eneo la kata ya Tanga lililopo ndani ya Manispaa ya Songea.

Akizungumza kabla ya makabidhiano ya eneo hilo, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Generali Balozi Wilbert Ibuge alisema ujenzi wa chuo hicho utasaidia kuleta maendeleo pamoja na kukuza uchumi wa Mkoa wa Ruvuma.

Aliongeza kuwa eneo hilo ambalo limekaa kimkakati kutokana na kuzungukwa na maeneo muhimu kiuchumi ikiwemo na stendi kuu ya mabasi ya Tanga, machinjio ya kisasa pamoja na Hospitali ya rufaa ya Manispaa ya Songea ambayo inatarajiwa kuanza kujengwa hivi karibuni.’Alibainisha’

Ibuge alisema miongoni mwa changamoto zilizopo katika eneo hilo ni pamoja na ukosefu wa huduma ya umeme pamoja na mawasiliano ambapo ametoa agizo kwa mamlaka husika kuhakikisha wanatatua changamoto hizo na kupeleka huduma hizo kwenye eneo husika.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha Uhasibu Arusha, Dkt Mwaitete Cairo alitoa shukrani kwa uongozi wa Halmashauri ya Mnaispaa ya Songea pamoja na Mkoa wa Ruvuma kwa kutoa eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho ambapo alisema kuwa ujenzi huo utaanza mara moja kwa kuzingatia mfumo wa kutumia ‘force account’ hivyo wananchi wajiandae kupata nafasi za ajira pamoja na kuwekeza miradi mbalimbali ambayo itasaidia kukuza uchumi na kuleta maendeleo binafsi na ya Mkoa kwa ujumla.

Akibainisha kuhusiana na mchakato wa ujenzi wa chuo hicho, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema eneo hilo lipo katika kata ya Tanga, mtaa wa pambazuko ambalo limetolewa bure na Manispaa kwa lengo la kutatua changamoto ya ukosefu wa Taasisi za elimu ya juu katika Mkoa wa Ruvuma.

Aidha, Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ametoa shukrani kwa uongozi wa chuo cha uhasibu Arusha kwa kukubali kujenga tawi la chuo hicho ambapo wamejibu kilio cha wananchi kuhusu upatikanaji wa Taasisi za elimu ya juu Mkoani Ruvuma.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Songea Hamis Abdallah Ally ametoa rai kwa wananchi kutoa ushirikiano katika kufanikisha ujenzi wa chuo hicho kama walivyotoa ushirikianokatika utekelezaji wa miradi mingine iliyopo ndani ya kata ya Tanga.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa