• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DAWA ZA MINYOO KUTOLEWA KWA WANAFUNZI 53962 - MANISPAA YA SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: March 17th, 2021

Manispaa ya Songea ni miongoni mwa Halmashauri nane 8 zilizopo  Mkoani  Ruvuma ambazo zinatekeleza zoezi la umezeshaji dawa za minyoo  kwa wanafunzi wa shule za msingi 93 zilizopo Manispaa ya Songea ambapo zoezi hilo  litaendeshwa na Walimu wa afya chini ya usimamizi wa  Wataalamu wa afya linalotarajia kufanyika tarehe 18 machi 2021.

Katika kufanikisha zoezi hilo Manispaa ya Songea imetoa mafunzo kwa walimu wakuu wa shule za Msingi 93, walimu wa afya 93 kutoka kila shule,   wenyeviti wa mitaa 95,  na watendaji wa kata 21 yaliyofanyika 16 hadi 17 machi 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi  kipaumbele Manispaa ya Songea  Broady Komba alisema jumla ya washiriki wa mafunzo 186 ambao ni walimu wa shule za msingi Manispaa ya Songea wamepewa mafunzo kwa ajili ya kusimamia zoezi la kuwamezesha wanafunzi dawa za kutibu  minyoo ya tumbo ambalo linatekelezwa chini ya Wizara ya Afya kwa magonjwa ambayo yamekuwa hayapewi kipaumbele.

Broady alisema mwaka 2021 shule 30  kati ya shule 93 zilizopo Manispaa ya Songea zilifanyiwa utafiti kwa wanafunzi  1548 wa darasa la kwanza na la pili ambao walichukuliwa damu na kupimwa kuangalia kama wanavimelea vya wadudu wa matende na mabusha,  na baada ya vipimo kufanyika  utafiti  ulionyesha kupungua kwa kiasi kikubwa cha vimelea vya wadudu  wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Alieleza kuwa mwaka 2021 dawa itakayotolewa kwa wanafunzi ni aina moja tu ambayo ni ya dawa Albendazole- dawa za minyoo ya tumbo ambayo humezwa kidonge kimoja tu na unashauriwa kula chakula kabla ya kumeza dawa hiyo.

Aliongeza kuwa dawa za kinga tiba ni salama na hazina madhara  endapo  zitatumika  kwa usahihi japokuwa yapo baadhi ya maudhi madogomadogo yanayoweza kutokea lakini hayana madhara na ni ya muda mfupi ikiwemo na kichefuchefu, kuharisha, kichwa kuuma, homa, na maumivu ya tumbo.

Alisema maudhi haya yanatokana na uwepo wa  vimelea vya magonjwa hayo mwilini ambapo unashauriwa kunywa maji mengi, au kutumia dawa za kutuliza maumivu endapo kama zitahitajika. Hivyo amewataka viongozi wa serikali za mitaa kutoa elimu kwa wazazi / wananchi juu ya utoaji wa chakula kwa watoto wao kabla ya kumeza dawa.

Aliongeza kuwa yapo Manufaa ya dawa za kinga tiba endapo zitatumika kwa usahihi ikiwemo na kupunguza maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, kuua vimelea vya magonjwa hayo, kuepusha upungufu wadamu, kupunguza magonjwa ya ngozi, kuboresha nguvu kazi pamoja na kuwafanya watoto wakue vizuri.

Naye mratibu  wa Elimu wa Afya Manispaa ya Songea Happiness Shenkunde alisema  kwa mwaka  2021 Manispaa ya Songea inatarajia kutoa dawa za minyoo ya tumbo kwa wanafunzi 53962 kati ya wavulana  26758 na wasichana 27204.

Shenkunde amewataka walimu hao kusimamia zoezi hilo kwa weredi na kuzingatia maelekezo yote yaliyotolewa na wataalamu wa Afya na kuhakikisha wanafunzi walioandikishwa wote wenye umri kuanzia miaka 5 hadi 14  wanapewa dawa za kinga tiba.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

17.03.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa