• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC Nyasa aweka jiwe la msingi mradi wa maji

Tarehe ya kuwekwa: August 13th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabela Chilumba hivi karibuni ameweka jiwe la msingi katika Mradi wa Maji  unaotekelezwa katika Kijiji cha Liparamba Kata ya Liparamba, Wilayani Nyasa ambao utawanufaisha wakazi 4694. Mpaka kukamilika kwake.

Katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi uliofanyika katika viwanja vya Kituo cha Afya cha Liparamba Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabeba Chilumba alimuagiza Mkandalasi anayetekeleza mradi huu kukamilisha kwa wakati na kuhakikisha maji yanatoka kabla ya mwezi wa tisa kama mkataba unavyosema.pia aliwaagiza wananchi waitunze miundombinu inayojengwa na Serikali kwa ajili ya kutatua kero ya maji iliyowasumbua kwa muda mrefu.

Aliongeza lengo la Serikali ni kutatua kero zinazowakabili wananchi wake ili waweze kufanya shughuli za kimaendeleo kama alivyohakikisha kata ya Liparamba inapata maji safi na salama.

“Nakuagiza Mkandarasi wa mradi huu ufanye kazi kwa juhudi usiku na mchana na ifikapo mwezi Septemba uwe umemaliza na maji yatoke ili yatatue kero kwa wananchi wa kata hii ya Liparamba.Pia ninawaagiza wananchi muitunze miundombinu ya maji kwa kuhakikisha jumuiya za watumia maji zinatekeleza majukumu yao”

Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya mradi huo,Kaimu Meneja wa wakala wa maji mijini na vijijini JosephatKayumba alisema mradi umefikia asilimia 85 ya utkelezaji na unatekelezwa na Mkandarasi  wa kampuni ya Ovansi Contruction Limited, iliyoshinda Zabuni ya kujenga mradi, kwa gharama ya shilingi (1,020,089,315.00) ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sekta ya maji awamu ya pili , (WSDP II) Nchini Tanzania ambao ulianza kutekelezwa mwaka wa fedha 2015/2016.

Alizitaja kazi zilizofanyika kuwa, ni kujenga miundombinu ya vyanzo  viwili vya maji (intakes) na sehemu moja ya kukusanyia maji, kujenga tanki la kutunzia maji lenye ujazo wa mita sabini na tano (75m3) na Mtandao wa mabomba, ya kusambaza maji kilometa ishirini na tano (25.85) .Pia amejenga vituo vya kuchotea maji ishirini na tisa(29) na matanki madogo ya kupunguza msongo wa maji katika bomba sita (6)chemba thelathini na saba (37) katika maeneo mbalimbali ya mradi, pamoja na alama za bomba.

.

Wananchi wa kijiji cha Liparamba, wamefurahi kutatuliwa kero ya maji kwa kuwa awali walikuwa wakitembea umbali wa kilometa takribani tano kufuata maji huduma ya maji  . kituo cha afya kilikuwa hakina maji hali iliyokuwa inawapa shida wagonjwa na wauguzi kutafuta maji wapatapo changamoto ya kuugua au kuuguliwa.   Kwa sasa wanaipongeza Serikali kwa kuwatatulia kero  ya maji katika kijiji chao.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kata ya Liparamba Diwani wa Kata hiyo Ditram Nchimbi aliishukuru Serikali kwa kutatua kero ya maji katika kata hiyo na kusema watahakikisha wanaitunza miundombinu  ya maji kwa kupanda miti rafiki maji na kuhakikisha vikundi vya watumia maji vinafanya kazi wakati wote.

“Mh Mkuu wa Wilaya tunaishukuru sana Serikali kwa kuhakikisha inatatua changamoto ya maji katika kijiji chetu kwa kuwa Wananchi walikuwa wakiteseka sana kutafuta maji kwa kuwa walikuwa wanatembea umbali wa Kilometa takribani tano kutafuta maji.Tutahakikisha tunaitunza Miundombinu kwa kuhakikisha jumuiya ya watumia maji zinafanya kazi muda wote”Alisema Nchimbi.

Serikali imetoa shilingi bilioni moja na nusu kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa maji katika kata ya Liparamba wilayani hapa ili kutatua changamoto ya maji iliyokuwa inawakabili wakazi hao.

Imeandikwa na Netho Credo

Afisa Habari Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa