• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC Songea ameitaka Jamii kupinga Ukatili wa Kijinsia

Tarehe ya kuwekwa: March 2nd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile  ameiasa jamii  kuwa na uwajibikaji  na malezi bora ya watoto  wao ili kupunguza au kuondoa ongezeko  la watoto  wa mtaani.

Alisema ili kuondoa matabaka na unyanyasaji wa kijinsia kwa jamii ni lazima kupambana kuondoa unyonge, na fikra   potofu  ili kuwa na Usawa na Haki.

Hayo yameinishwa katika uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani kuelekea siku ya kilele cha Maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka  ifikapo tarehe 08 Machi Duniani kote kwa lengo  la kukumbushana juu ya haki, usawa  kwa jamii hususani wanawake  kushiriki   katika kuchangia maendeleo,  yaliyofanyika katika uwanja wa Majimaji tarehe  01 Machi 2023.

Ndile  alisema lengo ni kutambua nafasi na mchango mwanamke katika kuchangia maendeleo ya jamii ambapo  amewataka wanawake  kujitokeza  kwa wingi katika kushiriki  kujiunga vikundi vya wajasiliamali ili kuweza kupata mikopo inayotolewa  na Halmashauri ya asilimia 10%  ili iweze kuwainua  kiuchumi  na kuongeza pato la familia.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Songea  Martin Mtani amesema  mikopo ya asilimia 4% ya fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya kuwezesha wanawake kiuchumi inaendelea kutolewa kila robo ya mwaka  kwa lengo la kujenga Tanzania ya viwanda.

Mtani aliongeza  kuwa katika kipindi cha julai  hadi Deisemba 2023 Manispaa ya Songea imetoa mikopo ya thamani ya Mil. 286,700,000 ambayo ni 10% ya mapato ya ndani iliyotolewa  kwa vikundi vya wanawake.

 Akibainisha baadhi ya changamoto ambazo zinawakabili wanawake  ni pamoja na familia kukosa malezi  bora kutokana na mvunjiko wa ndoa, mwamko duni wa wanawake katika kufanya shughuli za kiuchumi, pamoja ongezeko la watoto wanaoishi katika mazingira magumu

Ili kukabiliana na changamoto hizo Manispaa ya Songea inaendelea na utoaji wa elimu kwa jamii, wadau, kwa kupitia mikutano ya Serikali za mitaa, vikao mbalimbali, na vyombo vya Habari ili kuweka usawa katika jamii.

KAULI MBIU.

“UBUNIFU NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA CHACHU KATIKA KULETA USAWA WA KIJINSIA”

 

IMETOLEWA NA;

AMINA  PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.


Matangazo

  • MATANGAZO mbalimbali ya Manispaa ya Songea kwa njia ya Redio January 31, 2020
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Januari 2020 January 25, 2020
  • MATANGAZO muhimu kwa wakazi wa Manispaa ya Songea January 31, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MIAKA MIWILI YA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN " SONGEA MC "

    March 17, 2023
  • BIL 145.77 KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI MJI WA SONGEA.

    March 11, 2023
  • YALIYOJIRI SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MKOANI RUVUMA

    March 09, 2023
  • DC Songea ameitaka Jamii kupinga Ukatili wa Kijinsia

    March 02, 2023
  • Tazama zote

Video

BIL. 145.77 KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI MJI WA SONGEA
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa