• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC SONGEA AMEONGOZA MAOMBOLEZO YA KIFO CHA RAIS. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI.

Tarehe ya kuwekwa: March 27th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ameongoza maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe  Magufuli ambaye alifariki tarehe 17 machi 2021 na kuzikwa   26 machi 2021 Chato Mkoani Geita.

 Maombolezo hayo yamefanyika jana tarehe 27 machi 2021  na kuhudhuriwa na viongozi wa dini, wananchi wa Songea  yaliyofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Songea  ambapo  ni siku moja baada ya Baba yetu kulala katika nyumba yake ya milele.

Pololet alisema mnamo tarehe 17.03.2021 saa 5 usiku, aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassani alitangaza  kutokea kwa kifo cha Rais John Pombe Magufuli na kisha kutangaza siku 21 za maombolezo ya kifo cha kiongozi mkuu wa Taifa letu.

Alisema  lengo la kusanyiko hilo lilikuwa kwa ajili ya kuweka kumbukumbu na kufarijiana pamoja na kueleza sifa thabiti alizonazo mwanamapinduzi, mpenda Amani, na mtetezi wa wanyonge Hayati Dkt John Pombe Magufuli.

Alisema Taifa letu limepata msiba mkubwa ambao umetokea na ni kwa mara ya kwanza tumepata msiba wa Rais kufariki  akiwa madarakani japo kuwa tumewahi kupata msiba wa Rais wastaafu wawili ambao ni Hayati Mwl Julius Nyerere na Hayati Benjamini  Mkapa.

Alisema nanukuu “tunatambua kuwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassani amekuwa na uzoefu mkubwa sana katika shughuli za Serikali kuanzia akiwa mjumbe wa baraza la wakilishi Zanzibar, akiwa Waziri Serikalini kwa nafasi mbalimbali nchini, kuanzia 2015 aliteuliwa na hayati Dkt. John Pombe Magufuli kuwa mgombea mwenza na hatimaye kuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo alifanya kazi na Rais John Pombe Magufuli mpaka umauti ulipomchukua na kwa mujibu wa katiba aliapishwa na kupokea madaraka na kwasasa yeye ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”. Alisema Pololet.

Amewatoa hofu wananchi wa Songea,” amelala mtetezi wa wanyonge lakini yupo jemedali ambaye alikuwa msaidizi wake mkuu ndiye atakwenda kusimamia mipango yote ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi”. Alisema Serikali bado ni ileile ambayo ni Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa sita ambaye ni Samia Suluhu Hassani.

Naye mchungaji wa kanisa la KKKT Songea Mjini  George Kihegulo alisema “ tunaamini ya kwamba mungu amemuita na tunamuomba mungu ampumzishe kwa Amani mara ya baada ya kulitumikia Taifa hili.

Naye Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Shabani  Kitete  amewataka wanaruvuma na Taifa kwa ujumla kumkumbuka Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa mema yote aliyofanya akiwa hai na kuachana na matamshi mabaya  kwa Marehemu kwani vitabu  vitakatifu vimekataza, hivyo tunapaswa kuendelea kumuombea Dua na Sala  ili marehemu apumzike kwa Amani.

Naye Naibu Meya Manispaa ya Songea Jeremia Mirembe amewataka wananchi wote kuendelea kufanya maombolezo hadi 07.04.2021 kama Serikali ilivyotangaza, kupitia hilo ametoa rai kwa wananchi wa Songea kuachana na tabia ya kupiga miziki  kwenye kumbi za starehe na meaneo yote ya makazi ya watu bali kwasasa wanapaswa kuweka nyimbo za maombolezo ili kuungana na Serikali katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo ya kifo cha Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

INNALILLAH WAINAILAIHI RAJIUUN. (PUMZIKA KWA AMANI).

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

27. 03.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa