• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC SONGEA ATOA MAAGIZO KWA WEO'S NA MEO'S.

Tarehe ya kuwekwa: November 27th, 2020

“Songea tunasonga mbele”

Kauli hiyo imetamkwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema katika kikao kazi na wakuu wa Idara, Maafisa Watendaji wa Kata, Maafisa Watendaji wa Mitaa kwa ajili ya kupanga mkakati wa kumaliza kugawa vitambulisho  vilivyobakia 8873 vya wajasiliamali wadogo, kilichofanyika leo 27.11.2020 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Kamando alisema “kwa mwaka 2019 Manispaa Ilipokea vitambulisho vya ujasiliamali wadogo 11,000 ambavyo kwa jitihada nzuri za watendaji hao  waliweza kukamilisha kuvigawa kwa wakati nakuifanya  Halmashauri ya Manispaa ya Songea iwe ya kwanza kimkoa wa Ruvuma kwa utekelezaji mzuri” aliwapongeza.

Aliongeza kuwa mwaka huu 2020 Manispaa imepokea Vitambulisho 11,000 ambapo hadi hivi sas vitambulisho vilivyogawiwa ni 2127, ambavyo havijagawiwa ni 8873 ambapo amesema haoni sababu ya msingi ya kutomaliza kutekeleza zoezi hilo.

Amewataka wataalamu hao kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha kila mkuu wa Idara na Vitengo, Maafisa wa Watendaji kata na mitaa wanasimamia na kushiriki kwenye  zoezi hilo kikamilifu ili kufikia lengo lilikubalika.

Amewataka wataalamu hao kufanya kazi kwa kushirikiana (timu), na bila kuwanyanyasa  wajasiliamali hao ili kufanikisha zoezi la ugawaji wa vitambuliusho kwa wajasiliamali wenye sifa.

Lengo kuu la Serikali kuwawezesha wajasiliamali wenye mitaji midogo kukuza mitaji yao kwa kuondoa ushuru wa shilingi mia nne 400 ambao hutozwa kila siku na kulipa shilingi elfu ishirini 20,000 ambayo hulipwa mara moja ndani ya  mwaka husika. Pololet alibainisha.

Naye Afisa biashara Manispaa ya Songea Furaha Mwangakala alisema miongoni mwa mikakati waliyojiwekea ili kufikia lengo ni pamoja na kufanya kazi kwa timu na kwa kushirikiana na wakuu wa idara na vitengo, kila mtendaji wa kata /Mtaa kuhakikisha anashiriki zoezi hilo, pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa jamii umuhimu wa kununua  kitambulisho cha mjasiliamali.

Amewataka wataalamu hao kuanza kazi mara moja  ya ugawaji wa vitambulisho pamoja na kufanya  uhakiki kwa kila mjasiliamali kama ana kitambulisho cha ujasiliamali na kama hana kitambulisho anapaswa kununua kitambulisho au  kukata leseni ya biashara.

MTAYARISHAJI; 

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

27.11.2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa