• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ELIMU itolewe kwa Jamii kutokomeza ugonjwa wa ukoma

Tarehe ya kuwekwa: July 5th, 2018

Mwandishi wa Habari raia wa Ufaransa, Raoul Follereau alitumia muda wake mwingi kuzunguka dunia kueleza hali duni ya maisha ya watu walioathirika na ugonjwa wa ukoma.Kutokana na athari za ugonjwa wa ukoma jamii inatakiwa kuweka kipaumbele kwa kuwapatia huduma stahiki wagonjwa wa ukoma na watu walioathirika na ukoma.

Ugonjwa wa ukoma umekuwa ukiogopwa  kutokana na kusababisha ulemavu wa kudumu mwilini na kufanya waathirika kuwa tegemezi,ombaomba na kutothaminiwa katika jamii inayowazunguka.Katika Mkoa wa Ruvuma,tangu  mwaka 1917 wakoloni waliweka eneo maalum katika kisiwa cha Lundo kilichopo ziwa Nyasa,kwa ajili ya kuwatunza watu waliokuwa na ugonjwa wa ukoma kutokana na ugonjwa huo kusababisha ulemavu wa miguu na mikono hivyo kushindwa kufanya kazi za uzalishaji mali.

Tanzania ni miongoni mwa nchi 17duniani ambazo bado zina viwango vya juu vya ugonjwa wa ukoma. Mwaka 2013 Tanzania ilisaini makubaliano katika mkutano uliofanyika Bangkok Thailand yalioazimia kuwa na dunia bila ugonjwa wa ukoma.Miongoni mwa changamoto zinazotajwakuchelewesha kutokomeza ugonjwa wa ukoma ni jamii kuendelea kushikilia imanipotofu juu ya ukoma na wagonjwa kuchelewa kujitokeza kupata matibabu hadiwanapopata ulemavu.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu anasisitiza kuwa ukoma bado upo hapa nchini hivyo ni wajibu wa kila mdau kukabiliana nao.Hata hivyo Mwalimu anabainisha kuwa takwimu zinaonesha kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kutokomeza ugonjwa huo  kutoka kiwango cha utokomezaji cha watu 0.9  kati ya watu 10,000 mwaka 2006 na kufikia kiwango cha watu 0.4 kati ya watu 10,000 mwaka 2015.

“Kwa maana  nyingine katika kila watanzania 10,000 kiwango cha watu wenye ugonjwa wa ukoma sasa ni watu 0.4 mwaka 2015 kutoka wastani wa wagonjwa 0.9 katika watu 10,000 mwaka 2015. Haya ni mafanikio makubwa sana kwa sababu kiwango cha kimataifa cha utokomezaji ukoma kinatakiwa  kuwa chini ya mgonjwa mmoja katika watu 10,000’’,anasisitiza Mwalimu.

Anaitaja mikoa na wilaya ambazo zina wagonjwa wengi wa ukoma kuwa ni Lindi (Lindi Manispaa, Liwale, Lindi na Ruangwa),Morogoro (Halmashauri ya Ulanga, Kilombero na Mvomero), Dar es Salaam (Manispaa ya Temeke na Kigamboni) na  Tanga ( Halmashauri za Muheza, Mkinga  na Pangani).Mikoa mingine ni  Mtwara (Halmashauri ya Nanyumbu na Newala),Rukwa (Halmashauri ya Nkasi),Pwani (Halmashauri ya Rufiji na Mkuranga), Geita (Halmashauri ya mji Geita na Halmashauri ya Chato), Tabora (Halmashauri ya Sikonge), Mwanza (Halmashauri ya Kwimba na Misungwi), na Ruvuma (Halmashauri ya Songea na Namtumbo).

Anatoa rai kwa Mikoa na halmashauri hizo kuongeza juhudi za ziada na kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa wa ukoma kabla ya mwaka 2030 kama yalivyo malengo ya maendeleo endelevu ya dunia.

Mwandishi wa makala haya ni Albano Midelo

Mawasiliano yake ni albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa