• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

EPZA YAANZA KULIPA FIDIA KWA WANANCHI 955 KATA YA MWENGE MSHINDO

Tarehe ya kuwekwa: August 17th, 2023

EPZA imetenga fedha shilingi  Bil. 5.3 kwa  ajili ya kulipa fidia kwa Wananchi 955 wa Kata ya Mwengemshindo,  kwa lengo la kupisha maeneo yatakayotumika kwa ajili ya uwekezaji wa mradi wa EPZA.

Mamlaka ya EPZA kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Songea iliendesha zoezi la ulipaji wa fidia kwa awamu ya kwanza katika eneo la Mwengemshindo kuanzia tarehe 08/6/2015 hadi tarehe 19/06/2015. Katika zoezi hilo wananchi wapatao 1,183 (kati ya 2,149) walipaswa kulipwa fidia kiasi cha Sh.       1,926,866,730/= baada ya viwango vya fidia kuhuishwa kwa kuongezwa riba ya 8% kwa mujibu wa sheria ambapo hadi kufikia tarehe 19/06/2015 wananchi wapatao 1,130 walichukua hundi zao.

Aidha, kati ya wananchi 1,183 ambao malipo yao yalitayarishwa, wananchi 53 waliostahili kulipwa Sh. 31,215,492 hawakuchukua hundi zao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutojitokeza wakati wa zoezi la malipo na wengine kutokamilisha taratibu na nyaraka za mirathi kwa wakati kwa hundi zilizoandikwa kwa jina la marehemu ambao ndiyo walishiriki katika zoezi la uthamini hata hivyo Wananchi 966 hawakulipwa fidia katika awamu ya kwanza ambapo  kwa mujibu wa  uthamini uliofanyika mwaka 2009 jumla ya fidia yao ilikuwa Tshs. 2,024,319,947, pia  Kwa mujibu wa sheria kiwango hiki kinapaswa kuhuishwa kwa kuongezwa riba ambayo inayopaswa kuongezwa (compounding interest) kwa kipindi hiki ni 7%.

 Aidha, Wananchi 11 kati ya 966 ambao hawakulipwa fidia awamu ya kwanza,  walilipwa mnamo tarehe 01 Februari, 2023 baada ya kuchukua baadhi ya eneo lenye  ukubwa wa ekari 300 ndani ya eneo la Ruvuma SEZ kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ambayo inaeendelea kujengwa na kubaki  jumla ya Wananchi 955 ndiyo ambao hawajalipwa hadi sasa.

Hayo yamejiri kwenye mkutano wa Wananchi wa kata ya Mwengemshindo wakati wa ufunguzi wa  malipo ya  fidia ya ardhi, mimea, Nyumba au mashamba uliofanyika tarehe 16 julai 2023 katika ofisi ya kata ya Mwengemshindo ambao ulihudhuriwa na wananchi, EPZA pamoja na wataalamu mbalimbali kwa lengo la kuweka  uwazi na usawa katika ulipaji wa fidia kwa wananchi wa kata ya Mwengemshindo.

Akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanal. Laban Thomas “ amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani, Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt. Damas Ndumbaro, Diwani wa Kata ya Mwengemshindo pamoja na Vyama vya Siasa   kwa  usimamizi na ufuatiliaji wa suala hilo ambalo lilikuwa kero kwa wananchi wa kata ya Mwengemshindo.”  Alipongeza”

Alisema Malipo haya yalitakiwa kulipwa mwaka 2015 lakini kutokana na kutolipwa kwa wakati malipo hayo  yameongezeka kwa asilimia 7% ambayo yatalipwa kwa  mwananchi 955 kwa Ekari 5000 ambao tayari wamehakikiwa.

Kanal. Laban amewataka wananchi kutumia vizuri fedha hizo bila kuvunja mahusiano ndani ya familia ambayo  yanaweza kusababisha  mfarakano  katika familia.

Ametoa wito kwa wananchi na wataalamu wa Manispaa ya Songea kuhakikisha wanafanya usafi wa mazingira kila wakati pasipo kusubili usafi wa kila mwisho wa Mwezi ili kuweka mji katika hali ya usafi.

Amewataka wananchi kutoa lishe bora kwa watoto chini ya miaka mitano, akina mama wajawazito na jamii kwa ujumla ili kuwa na jamii yenye afya bora pamoja na kila mwananchi ambaye hajajiunga Mfuko wa Bima ya Afya ahakikishe anajiunga ili kupata matibabu yenye uhakika katika vituo mbalimbali vya afya.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile alisema” EPZA  ni Mamlaka ya maeneo maalumu  ya uzalishaji  kwa mauzo ya nje ambao huwekeza katika maeneo  kwa ajili Uwekezaji wa barabara, na viwanda  ambapo Serikali imechukua maeneo ili kujenga viwanda  vikubwa vitakavyowezesha kuongeza ajira  katika jamii.

Akizungumza mwakilishi wa EPZA Wilson Malosha alisema “ Serikali sasa iko tayari kulipa wananchi ambao hawakulipwa katika wamu ya kwanza ambapo  zoezi la uhakiki lilianza  tarehe 3 Agosti, 2023 hadi tarehe 10 Agosti ambalo limefanikiwa kupata takwimu sahihi ambapo wananchi 803 kati ya 955 wanaanza kulipwa huku  zoezi la uhakiki bado linaendelea ili kukamilisha idadi ya wananchi waliobaki 152 ambao bado hawajahakikiwa.

Ametoa rai kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano  katika kufanikisha zoezi hili la ulipaji ili kila mmoja apate stahili zake na kupisha maeneo kwa ajili ya kuanza uendelezaji ambao utawezesha  kupata Wawekezaji kwa ajili ya maendeleo ya taifa kwa ujumla. 

Kwa upande wa wananchi wa kata ya Mwengemshindo wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kufanikiwa kulipa fidia ya ardhi ambayo ilikuwa ni kero kubwa kwa wakazi wa kata ya Mwengemshindo.  “ Wananchi wameshukuru.”

IMEANDALIWA NA;       

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI. 








Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa