• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

FAHAMU kuhusu viashiria vya udanganyifu

Tarehe ya kuwekwa: July 2nd, 2018

UDANGANYIFU ni tendo lolote la uamuzi au uasi unaofanywa kwa lengo la kuwadanganya wengine na kusababisha anayedanganywa kupata hasara na anayedanganya kufaidika ama kwa kupata fedha.

Akitoa mada ya vihatarishi vya udanganyifu kwa madiwani,wataalam na maafisa watendaji wa mitaa na Kata wa Manispaa ya Songea katika mafunzo ya siku mbili,Mkaguzi wa Ndani wa Manispaa hiyo Joel Mantakara anasema tendo la udanganyifu hujumuisha wizi,rushwa na njama.

Ametahadharisha kuwa hapa nchini mashirika na Taasisi zote zinakabiliwa na hatari za udanganyifu ambapo udanganyifu mkubwa umesababisha kuanguka kwa mashirika katika kufanya biashara.

Mantakara ametolea mfano Kampuni ya kimataifa ya ENRON ambayo ilikuwa inafua umeme huku Taxes nchini Marekani mwaka 2001 Kampuni hiyo ilianguka katika biashara kutokana na udanganyifu uliokuwa unafanywa na viongozi wa kampuni hiyo katika hesabu zao zikionesha Kampuni inapata faida.

“Viongozi hao walihamasisha wawekezaji waendelee kuwekeza katika Kampuni hiyo wakati katika hali halisi Kampuni ilikuwa inapata hasara katika kiwango cha kutisha hivyo kufikia mwaka 2001Kampuni ilianguka’’,anasema Mantakara.

Anabainisha zaidi kuwa kutokana na udanganyifu,kashfa kubwa zimekuwa zinazikumba Kampuni,Taasisi na mashirika mbalimbali duniani hali ambayo imelazimisha Kampuni zenyewe,mashirika na watu binafsi kuanza kuchukua hatua dhidi ya udanganyifu na ulaghai ili usiendelee kufanyika baada ya kuweka misingi ya kuzuia udanganyifu.

Kwa mujibu wa Mkaguzi huyo wa Ndani wa Manispaa ya Songea,sababu zinazosababisha kuwepo kwa viashiria vya uganganyifu  anazitaja kuwa ni mazingira ambayo Taasisi inayafanyia kazi,mfumo wa udhibiti wa ndani na maadili ya Kampuni na maadili ya wafanyakazi.

Hata hivyo Mkaguzi huyo anaeleza kuwa udanganyifu umegawanyika katika maeneo makuu matatu ambayo ni  udanganyifu ambao unaweza kufanyika katika taarifa za fedha na udanganyifu unaoweza kufanyika kutokana na matumizi ya rasilimali za Taasisi.

Maeneo mengine ya udanganyifu ni udanganyifu ambao unaweza kufanyika kutokana na rushwa na kukosa maadili na udanganyifu wa ndani ya Taasisi unaohusiana na ajira.

“Mtu yeyote yupo kwenye nafasi ya kuweza kufanya udanganyifu au ulaghai na wakati mwingine watu wanaoweza kufanya ulaghai,wanaweza kuwa katika nafasi kubwa za kazi na wanaheshimika katika jamii na wana maadili mema.wanaweza kuwa viongozi waandamizi,wa kati na wa chini’’,anasisitiza Mantakara.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Juni 2,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa