• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

FAHAMU MAFANIKIO BAADA YA UHURU "SONGEA"

Tarehe ya kuwekwa: December 10th, 2022

“Maadhimisho ya siku ya Uhuru  9 Desemba yatumike  kwa kuelimisha jamii katika kuhifadhi  tunu iliyowekwa na Wazee wetu.”

Kauli hiyo imetamkwa katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru 9 Desemba ambayo ilifanyika kiwilaya katika Ukumbi wa Manispaa ya Songea iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka Zanzibar, wataalamu, na viongozi kutoka Halmashauri ya Madaba, Songea Vijijini, na Manispaa.

Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Songea ambaye aliwakilishwa na Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ambaye alisema “Lengo la maadhimisho haya ni kufanya Tafakuri na kukumbuka wapi tulipo na wapi tunatoka  ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ambayo inamtaka kila mwananchi  kulinda uhuru wetu.”

Mhe. Mbano alibainisha kuwa jukumu la kulinda Uhuru ni la kila mmoja wetu  kwa kuwa Uhuru unalindwa kwa kufanya kazi  kwa maana changamoto za Mtanzania zitatatuliwa na Mtanzania mwenyewe, hivyo amehimiza wananchi kuwa na  Uzalendo kwa maendeleo ya Taifa.

Maadhimisho hayo yamefanyika kwa Mdahalo ambao ulizungumzia  masuala ya Siasa na Uongozi, Elimu na Afya, Miundombinu, Mahusiano, na Nishati, Biashara, viwanda na uwekezaji, kilimo na mifugo, Maji na Mazingira.

Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea  Dkt. Frederick Sagamiko amewataka wananchi kuwa na utamaduni wa kupenda kujisomea historia ambayo itasaidia kukumbuka utamaduni wa maisha yetu ambao inaonesha watu walio  wengi hupenda kufundishwa  sio kujifunza.

Dkt. Sagamiko aliongeza kuwa nanukuu “ kuna mambo mengi sana yanakwenda kupotea kutokana na tabia yakutokuwa na utamaduni wa kufuatilia uhalisia wa kabla ya uhuru ambao jamii  imekariri baadhi ya matukio muhimu  ya kitafa  ya kihistoria kama upatikanaji wa maji, viwanda.”mwisho wa nukuu.

Alisema  hapo awali huduma hazikuwa nzuri kutokana na kutawaliwa na waingereza ambapo walitutumia kwa lengo la kuwatumikia wao  katika kuzalisha mali  hali ambayo hupelekea jamii kutopenda vitu vitokanavyo na asili yetu hali  inayosababisha  kuuwa viwanda vya ndani.” Alibainisha”

Hivyo ametoa Rai kwa wananchi wa Songea kuelekea maadhimisho yajayo ya  62  mwaka 2023 kuwepo kwa Makala inayoelezea  maisha yetu kabla ya Uhuru na baada ya uhuru ambapo itasaidia kuweka kumbu kumbu katika maandishi ili kulinda historia  na kurithisha  kizazi kijacho. Dkt. Sagamiko alisisitiza.

Alibainisha kuwa kwa Manispaa ya Songea mara baada ya Uhuru imefanya shughuli nyingi sana ikiwemo na kuboresha miundombinu ya barabara za mitaa, miundombinu ya shule za msingi na Sekondari, UJenzi wa masoko mawili ya kisasa (Manzese) ambayo yanatarajia kutangazwa kwa ajili ya kuanza ujenzi hivi karibuni, ujenzi wa chuo kikuu cha hesabu (Arusha) ambapo imetengwa shilingi Bil. 17, Maji, Umeme, na Stendi kuu ya Mabasi Songea, ujenzi wa kiwanda kidogo Lilambo,  ujenzi wa barabara wa kiwango cha Lami km 10.5 katika kata Mfaranyaki, Majengo, Misufini na Mjini naujenzi wa hosptali ya Rufaa ya Mkoa, Ujenzi wa vituo vya afya, ujenzi wa hosptali ya Wilaya iliyopo kata ya Tanga na  nyinginezo. 

Aliongeza kuwa Jukumu la Serikali ni kuweka miundombinu wezeshi kwa wafanyabiashara hususani  katika kuwapanga wamachinga na sio dhamira ya Serikali  kuuwa biashara bali Serikali  inalenga kuwaweka huru   wafanyabiashara  wadogo.

Amewataka Maafisa watendaji wa kata na Mitaa kuwepo kwenye maeneo yao ya kazi na kuhakikisha wanasimamia zoezi la kuwapanga wamachinga kuwepo kwenye maeneo rasmi yaliyopangwa  na Halmashauri.


Naye  Juma Nyumayo (MDAU) alisema  Uhuru ni hali  au uwezo wa kujitawala au uwezo wa kutekeleza majukumu, kufanya maamuzi ya kushughulikia masuala yako wewe/ yenu bila kuwa chini ya Mamlaka nyingine.

Nyumayo aliongeza kuwa  Mifumo ya Sheria za wakoloni  za makosa jinai, ambazo hutumika  Tanzania zilipokelewa kutoka kwa Waingereza pamoja na Mifumo ya Mahakama.

Naye Furaha Mwangakala  alisema kabla ya uhuru Wilaya ya Songea  hatukuwa na kiwanda, Soko, na Uwekezaji ambapo biashara nyingi  zilifanywa na wageni kwa kuchukua bidhaa na kubadilishana  bidhaa kwa bidhaa.

 Mwangakala aliongeza kuwa Kabla ya uhuru Wilaya ya Songea ilikuwa  na maduka mawili 2 ambapo baada ya uhuru Wilaya ya Songea ina jumla ya  wafanyabiashara  14,260 kati ya hao wafanyabiashara wakubwa 3360 na wafanyabiashara wadogo ni 10,700.

Naye Afisa Mazingira  Beno Philipo  alisema Huduma ya maji Manispaa ya Songea ilianza mwaka 1950 kabla ya uhuru ambapo wakati Nchi inapata Uhuru 1961 chanzo kikuu cha maji kilikuwa Mto Ruvuma ambacho kililenga kutoa huduma ya maji kwa wakazi 3000 kwa mahitaji ya maji  lita 400 kwa siku.

Beno aliongeza kuwa kuongezeka kwa wakazi wa huduma ya maji kutoka 5000 kwa mwaka 1961 hadi 236,936 sawa na asilimia 88% ya wakazi wote wa Songea ambao wanapata maji safi na salama.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa