• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

GESI asilia kuongeza Pata la Ndani la Taifa mara 15

Tarehe ya kuwekwa: June 11th, 2018

GESI asilia iliyogundulika Tanzania ikisimamiwa vizuri inaweza kuongeza pato la ndani la Taifa  (GDP) mara 15 ya pato la sasa hivyo  kuifanya Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi zenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Mtaalamu wa Raslimali za Taifa Kaiza Bubelwa anaishauri Serikali  ihakikishe inasimamia vizuri sheria ya gesi asili  ili iweze kudhibiti gesi asilia badala ya sekta hiyo kudhibitiwa na wawekezaji.

Anabainisha zaidi kuwa gesi asilia ikidhibitiwa na serikali itaongeza pato la ndani la Taifa mara 15 ya pato la sasa na kwamba makosa ambayo yamefanyika katika sekta ya madini ya kuwanufaisha zaidi wawekezaji kuliko wenye rasilimali yasirudiwe katika gesi asilia na mafuta.

 “GDP ya Tanzania mwaka 2011 ilikuwa ni  dola za Marekani bilioni  28.5,Kenya ilikuwa ni dola bilioni 34 ambapo gesi asilia pekee ikichimbwa na kusimamiwa inaweza kuongeza uchumi wetu  mara 15 ya GDP  ya sasa”,anasisitiza Bubelwa.

Bubelwa anasema nchi kwa miaka mingi  imeshindwa kunufaika na rasilimali zilizopo kutokana na kukosa usimamizi madhubuti wa rasilimali za madini katika hatua zote za kuanzia utafutaji,uchimbaji,usafirishaji,mikataba na kuweka, sera na sheria zitakazowanufaisha watanzania wote.

Hata hivyo serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk.John Magufuli imeonesha nia ya dhati katika kusimamia rasilimali za Taifa kwa kupitisha sheria za kusimamia rasilimali za nchi ili hatimaye sasa watanzania waweze kunufaika na rasilimali hizo ambazo tumezawadiwa na Mwenyezi Mungu.

Hata hivyo Bubelwa anataja mambo yaliyochangia watanzania kutonufaika na rasilimali zetu kuwa ni rushwa,upofu wa sheria,ukosefu wa utawala bora, kupotea na kutotumika kwa uwiano katika mfumo wa uchimbaji, maamuzi ya kuchimba na uwazi katika utoaji wa mkataba.

Carlos Mbuta ni Afisa Mkuu Mwandamizi wa Baraza la Taifa la Mazingira NEMC ametahadharisha kuwa rasilimali ya gesi asilia na mafuta ambayo inachimbwa,siku moja itakwisha hivyo ni lazima kufungua mifuko maalum  ya mapato ambayo itatumika kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.

Gesi asilia inatarajia kuanza kuzalishwa na kusafirishwa mwaka 2021.

Gesi asilia iligundulika kwa mara ya kwanza hapa nchini mwaka 1974 katika kisiwa cha Songosongo mkoani Lindi,ugunduzi mwingine ulifanyika mkoani Mtwara mwaka 1982 eneo la Mnazibay na ugunduzi bado unaendelea,lakini uzalishaji  wa gesi asilia ulianza mwaka 2004.

Afisa Mkuu Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini TPDC Mhandisi Modesto Lumato anasema jumla ya gesi asilia ambayo imegundulika nchini katika mikoa ya Lindi na Mtwara inafikia futi za ujazo zaidi ya trilioni 57 ambapo futi trilioni 30 zinatarajiwa kuuzwa nje ya nchi.

Mwanasheria na Mkurugenzi wa Chama cha Watetezi wa Mazingira Tanzania(LEAT) Dk.Nshala Rugemeleza anasisitiza kuwa Tanzania haina wataalamu wa kutosha ambao wanaweza kutuambia ukweli kuhusu madini,gesi na mafuta yaliopo nchini badala yake tunategemea wataalamu kutoka nje ambao wamekuwa wakitoa taarifa za udanganyifu kuhusu rasilimali zetu.

Nchi ya Norway  ambayo hivi sasa ina idadi ya watu wasiozidi milioni tano, inapata neema kubwa kutokana na sekta ya mafuta na gesi asilia.Mfuko ulioundwa kwa ajili ya kuweka fedha za rasilimali hizo katika nchi hiyo una zaidi ya Dola za Marekani bilioni 500 ambazo haijulikani zitatumika namna gani kutokana na mfuko kuwa na pesa nyingi.

Kwa uongozi tulionao hivi sasa chini ya Rais Dk.John Magufuli,rasilimali ya gesi asilia inaweza kuiondoa Tanzania katika nchi masikini duniani na kuiingiza kuwa nchi yenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Mwandishi wa Makala haya anaitwa Albano Midelo albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa