• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

GESI asilia kwenye magari ni nafuu ukilinganisha na mafuta

Tarehe ya kuwekwa: June 21st, 2018

UTAFITI umebaini kuwa matumizi ya gesi asilia kwenye magari yanaokoa asilimia 65 ya gharama ukilinganisha na matumizi ya mafuta hali ambayo imesababisha baadhi ya nchi duniani kutumia gesi asilia na kuachana na mafuta.

Baadhi ya nchi duniani zimeanza kutumia gesi asilia kwenye magari hali ambayo imeleta unafuu kwa wananchi na serikali za nchi hizo kutokana na ukweli kuwa gesi asilia kwenye vyombo vya moto ni nafuu ukilinganisha na mafuta.

Baadhi ya nchi ambazo zinazotumia teknolojia ya gesi asilia kwenye magari ni Afrika Kusini,Misri na Msumbiji.

Utafiti umebaini kuwa matumizi ya mfumo wa gesi asilia katika nchi zilizoanza kutumia umeokoa fedha nyingi za kigeni zinazotumika kuagiza nishati ya mafuta toka nje ya nchi  na kuokoa uharibifu wa mazingira kwa sababu gesi asilia haizalishi hewa ukaa ambayo ni hatari katika mazingira na afya.

Baadhi ya nchi zilizoendelea duniani ikiwemo Norway zinatumia gesi asilia kwa ajili ya kuendeshea magari ambapo takwimu zinaonesha kuwa magari  Zaidi ya milioni 11 duniani yanatumia gesi asilia na nchi inayoongoza ni Pakistan yenye magari milioni 2.1, ikifuatiwa na Argentina yenye magari milioni 1.8 Brazil yenye magari milioni 1.7.

Utafiti ambao umefanywa na wataalam wa gesi asilia unaonesha kuwa gesi asilia ikitumiwa wakati wote, injini ya gari itadumu zaidi kwa sababu haizalishi uchafu ikilinganishwa na petroli na kwamba kama mwenye gari alikuwa anabadili mafuta ya injini kila baada ya kilomita 3,000, mfumo wa kutumia gesi asilia utamwezesha kubadilisha  baada ya kilomita 6,000.

Joseph Mkinga Mhandisi ambaye amesomea shahada ya pili ya  uhandisi wa mafuta (Petrolium Engineering) nchini Norway  anasema nchi ya Norway imepiga hatua kubwa katika sekta ya mafuta na gesi ambapo hivi sasa ni miongoni mwa nchi kumi duniani zinazoongoza kwa uzalishaji wa gesi na mafuta.

Anabainisha kuwa katika nchi ya Norway mabasi yote ya abiria  yanatumia gesi asilia badala ya mafuta hali inayosababisha uchumi wa nchi hiyo kukua kwa kasi,serikali yake inasimamia vizuri rasilimali chache zilizopo katika mafuta na gesi asilia hivyo kuwaletea wananchi wake maendeleo endelevu .

Baada ya nchi hiyo  kugundua mafuta na gesi,serikali ilianza kuwasomesha vijana wake kuhusu gesi asilia na mafuta na wale wanafunzi wa kwanza waliokuwa wanahitimu  waliajiriwa kuwa walimu katika sekta ya gesi na mafuta.

Amesema katika nchi hiyo ambayo hivi sasa  inaongoza kwa kuwa na wataalam wengi katika sekta ya mafuta na gesi duniani baadhi yao wanafanyakazi katika nchi ambazo kuna mafuta na gesi ikiwemo Tanzania.

Nchi ya Norway  yenye watu wasiozidi milioni tano  ilikuwa nchi maskini hadi ilipogundua gesi na mafuta mwaka 1969, ilisimamia sekta hiyo kikamilifu ambapo hivi sasa  mfuko wa gesi na mafuta  katika nchi hiyo una zaidi ya dola bilioni 500.

 Kiasi hicho cha fedha katika nchi ya Norway kitatumika kizazi na kizazi hata kama gesi na mafuta yote katika nchi hiyo yatamalizika.Tanzania inatarajiwa kuwa nchi yenye uchumi wa kati mwaka 2025 baada ya gesi asilia kuanza kuzalishwa rasmi na kuuzwa nje ya nchi.

Kama kweli Tanzania imedhamiria kupata maendeleo makubwa katika sekta ya mafuta na gesi asilia ni vema kuwekeza kwa kuwaandaa wataalam wake  kabla ya gesi iliyogundulika kuanza kuzalishwa rasmi.

Hata hivyo juhudi za serikali kuanzisha kozi za mafuta na gesi zimeanza kuonekana baada ya kuanzisha shahada za gesi asilia na mafuta vyuo vikuu vya Dar es salaam na Dodoma tangu mwaka 2014.

Wataalam katika sekta ya gesi asilia na mafuta wakiwepo wa kutosha na serikali kuandaa sera,sheria,miongozo na kanuni bora za sekta ya mafuta na gesi  kama ilivyo katika nchi ya Norway  sekta hiyo itawanufaisha zaidi watanzania badala ya kampuni za kigeni hivyo kuwa na uchumi endelevu.

Mwandishi wa Makala haya ni Albano Midelo ambaye amesomea masuala ya mafuta,gesi,mafuta na mazingira mawasiliano yake ni albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa