• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALI YA UDUMAVU YAFIKIA WASTANI 42.9 KATIKA KANDA ZA NYANDA ZA JUU KUSINI.

Tarehe ya kuwekwa: August 8th, 2020

Hali ya udumavu katika Mikoa ya kanda za nyanda za juu kusini ni wastani wa 42.9 ambapo alisema kiwango hicho kipo juu ya wastani wa Taifa ambao ni 31.8 licha ya kuwa na uzalishaji mzuri wa chakula na kuwa na ziada kubwa ya chakula.

Kauli hiyo imetolewa leo 08/08/2020  kwenye kilele cha maadhimisho ya maonesho ya Nanenane yaliyofanyika katika uwanja wa John Mwakangale Jijini Mbeya.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Majaliwa Kassimu Majaliwa ambaye aliwakilishwa na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dr. Tulia Ackson .

Tulia alianza kwa kusema Mikoa ya kanda za  nyanda za juu kusini inaendelea kuzalisha mazao mengi  ya chakula ambapo kwa mwaka  2019-2020 uzalishaji wa chakula umekuwa tan Milioni 11,446,888.5 sawa na 91.4 kwa  lengo la kuzalisha tan milioni 12,522,929.8 ambazo kwa sasa hutoshelevu wa chakula ni ziada kwa wastani 201.

Aliongeza kuwa kutokana na changamoto kubwa  ya udumavu iliyojitokeza  aliwaagiza viongozi wakuu wa  Mikoa kukabiliana na hali hiyo ya udumavu pamoja na kufanya utafiti kujua sababu za kuwepo kwa  viwango vya juu vya udumavu na kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo.

Alibainisha kuwa  kutokana na changamoto ya uhaba wa maeneo ya malisho ya mifugo ambapo  hupelekea kutokea kwa migogoro kati ya Wakulima na Wafugaji  kutokana na kuwa na idadi kubwa ya mifugo ikiwemo ng’ombe 3266000, mbuzi 1378237, na kondoo 343586, katika kupunguza migogoro hiyo Serikali imeanza kuboresha safu ya mifugo ili kuwa na idadi ya Mifugo inayoendana na ardhi tuliyonayo.

Alisema kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri ya usafirishaji kwa kuboresha miundombinu ya Barabara na uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe ili kuwezesha ndege za mizigo kutua usiku na mchana.

Aliongeza kuwa Serikali imeanza kuweka mkazo maalmu wa kuendeleza ushirika kutokana na baadhi ya wakulima kukata tamaa kwasababu mbalimbali ikiwemo baadhi ya viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika kutotekeleza wajibu wao.  Hata hivyo alifafanua kuwa Serikali imeamua kuweka mkazo maalmu kwa mazao matano yaani chai, Kahawa, Korosho, Tumbaku na Pmba.

Kauli mbiu katika maadhimisho hayo ni: Kwa maendeleo ya Kilimo, Mifugo, na Uvuvi chagua viongozi bora 2020.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY,

KAIMU AFISA HABARI- MANISPAA YA SONGEA.

08/08/2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa