• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA YAJIPANGA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA, UMEME NA MAJI.

Tarehe ya kuwekwa: October 1st, 2021


Halmashauri ya Manispaa ya Songea imejipanga kutatua changamoto za miundombinu ya barabara, umeme na maji kwa wananchi wake.

Hayo yameelezwa katika kikao cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Songea kilichofanyika tarehe 30 Septemba 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi pamoja na wataalamu mbalimbali ndani ya Manispaa ya Songea.

Akiongoza kikao hicho Naibu Meya wa Manispaa ya Songea Jeremiah Milembe katika kipindi cha maswali na majibu ambapo Waheshimiwa Madiwani walieleza changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika maeneno yao hasa miundombinu ya barabara , umeme na maji ambapo miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na ubovu wa barabara za mitaa, ukataji wa umeme mara kwa mara pasipo kutoa taarifa maalumu kwa wananchi, kucheleweshwa kwa uingizaji wa umeme pamoja na ukataji wa maji kwenye maeneo mbalimbali bila taarifa.

Akijibu malalamiko hayo Mhandisi mipango TANESCO Mkoa wa Ruvuma Eng. Sosthenes Maganga alisema kuwa sababu zinazopelekea ucheleweshwaji wa miundombinu ya umeme kwenye makazi ya wananchi pamoja na taasisi za umma na binafsi ni ukosefu wa bajeti ya kutosha ili kukamilisha miradi hiyo na upungufu wa nguvu kazi.

Maganga ametoa rai kwa viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kutoa taarifa mapema TANESCO mara tu utekelezaji wa miradi unapoanza ili kurahisisha upelekaji wa miundombinu ya umeme mapema kwenye miradi hiyo.

Kwa upande wake kaimu meneja TARURA Manispaa ya Songea Dotto Magese amesema kuwa wamejipanga kutengeneza barabara zote zenye changamoto ndani ya Manispaa ya Songea pamoja na kuweka utaratibu maalumu wa kuwashirikisha viongozi hasa Madiwani wa eneo husika ambalo utengenezwaji wa barabara utakuwa unafanyika ili kuweza kupata maelekezo sahihi.

Naye Mkuu wa Wilaya wa Songea Pololet Kamando Mgema alipewa nafasi ya kuzungumza katika Baraza hilo na kuwataka Madiwani kuendelea kuhamasisha wananchi juu ya kupata chanjo ya UVIKO 19 hata kwa kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo yao.


IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

01.10.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa