• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI zote nchini zatakiwa kusimamia mapato

Tarehe ya kuwekwa: September 28th, 2018

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim M. Majaliwa (MB) ametoa rai kwa Madiwani, Wakurugenzi na Makatibu Tawala wa Mikoa  kubadilisha mtazamo  katika suala zima  la usimamizi, ukusanyaji na  utumiaji  wa fedha  zinazokusanywa kwenye Halmashauri zote nchini

Akifungua Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika leo katika ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete Jijini Dodoma. Mhe. Majaliwa amesema ustawi wa jamii unategemea uwezo wa mapato yake na matumizi yenye tija kwa fedha zinazokusanywa

Mhe. Majaliwa amefafanua kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha Halmashauri zinakuwa na uwezo wa kujitegemea kimapato kwa zaidi ya asilimia 80 ifikapo mwaka 2025 ili kutimiza lengo la Serikali katika Dira ya Maendeleo ya 2025.

Amesema kuwa Serikali ya awamu ya Tano imekuwa ikichukua  hatua mbalimbali  ili kuhakikisha dira ya maendeleo ya mwaka 2025 kwa kuanzisha  utaratibu wa kugharamia  miradi  ya kimkakati  yenye lengo  la kuziongezea Halmashauri mapato  ya uhakika  na kupunguza utegemezi  wa ruzuku  ya Serikali.

Mhe. Majaliwa amesema kuwa  hadi sasa Serikali  imeidhinisha shilingi bilioni 131.5 kutekeleza miradi ya  ipatayo 22 katika Halmashauri  17 zilizokidhi vigezo kwenye Mikoa 10 na mpaka sasa kiasi cha shilingi bilioni 16.4 zimepelekwa kwenye Halmasahauri  hizo kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa  miradi ya kimkakati.

Amaesema kuwa  uchambuzi wa miradi  mingine ya kimaendeleo  unaendelea na Halmashauri  zitakazokidhi vigezo zitapata fedha kwa  ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo na amezitaka Halmashauri zote nchini  kutumia fedha  hizo kwa ajili ya  malengo yaliyokusudiwa.

“ Serikali  haitakuwa  na utaratibu wa kutoa fedha bila kufahamu kwa kina fedha hizo zinakwenda kufanya nini na zinaleta mabadiliko gani kwa kuwa nimesikia kwamba katika baadhi ya Halmashauri fedha zilizokwishatolewa bado hazijaanza kutumika kikamilifu, nawaagiza Waheshimiwa Madiwani kusimamia matumizi ya fedha hizo ili Halmashauri  zipate miradi yenye ubora unaotakiwa na inayokamilika kwa wakati” Anafafanua Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amesema Serikali imeongeza ukusanyaji wa mapato  katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuhakikisha Halmashauri zote 185 zinatumia Mfumo wa ukusanyaji wa mapato wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na kufanya ongezeko la mapato kutoka shilingi bilioni 379 kwa mwaka 2014/2015 hadi kufikia  shilingi bilioni 553.39 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 .

Amewaonya Viongozi wa Halmashauri wanaolalamikia kutokuendelea kulalamika  kuhusu baadhi ya vyanzo  vya mapato  kuchukuliwa na Serikli  kuu bali  waongeze  bidii  na ubunifu  katika kutafuta  vyanzo vipya vya  mapato ili Mamlaka za Serikali za Mitaa  ziweze kujitegemea.

“Fanyeni kazi  ionekane, tusione Mamlaka  za Serikali za Mitaa ambazo kweli zinatoa huduma, tuone vyumba vya madarasa vinaongezeka, watoto hawakai chini, Zahanati zinazopendeza  hapo tunaweza  kusema sasa  Halmashauri zimekomaa” Amefafanua Mhe. Majaliwa

 Wakati huo huo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Mhe. Selemani Jafo amewaagiza Wakurungenzi wa Halmashauri kuacha kufanyakazi kwa mazoea bali wafanye kazi kwa bidii kwa kutumia weledi ili  kuleta mabadiliko katika utendaji kazi katika Halmashauri

Aidha Mhe. Jafo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kuwakopesha wanawake, vijana  na watu wenye ulemavu ili kuwawezesha kiuchumi  na kupunguza umaskini  nchini.

Imetolewa na tovuti ya TAMISEMI

Septemba 27,2018


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa