• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HOMA ya nguruwe tishio Songea

Tarehe ya kuwekwa: January 26th, 2018

UGONJWA hatari wa homa ya nguruwe umeingia katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ambapo hadi sasa zaidi ya nguruwe 100 wamekufa.

Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Rozina Chuwa amesema katika kipindi cha wiki mbili vimetokea vifo hivyo 100 vya nguruwe na kwamba hadi kufikia Jumapili iliyopita nguruwe 48 walikuwa wamekufa kutokana na ugonjwa huo.

Amesema ugonjwa huo unaonezwa virusi aina ya African Swine Fever Virus’ hauna kinga na unaenea kwa kasi kubwa katika Manispaa ya Songea yenye jumla ya nguruwe 4581 ambapo ametaja maeneo ambayo yanaongoza kuathirika na ugonjwa huo ni Lizaboni ambako nguruwe zaidi ya 100 wamekufa.

Maeneo mengine ambayo yameripotiwa kuingia ugonjwa huo Januari 24 na 25 mwaka huu ni Ruhuwiko, Mshangano na Mjimwema.

“Kwa kuwa ugonjwa wa homa ya nguruwe hauna kinga,kitaalam inashauriwa njia rahisi ya kukabiliana na ugonjwa huu ni kuchinja nguruwe ambao wapo katika maeneo ambayo umetokea ugonjwa huo ambao unaua nguruwe kwa kasi’’,anasisitiza Chuwa.

Hata hivyo amesema njia hiyo inakuwa ngumu kutekelezeka kwa sababu wananchi wengi hawakubali kuchinja nguruwe wao,hali ambayo inasababisha ugonjwa huo kuenea kutokana  na kununua nyama ya nguruwe wenye ugonjwa.

Amesema ugonjwa huo haina madhara kwa binadamu ambapo kitaalam nguruwe aliyekufa kwa ugonjwa huo anatakiwa kuzikwa katika shimo lililopuliziwa dawa lenye urefu wa zaidi ya meta moja.

“Sisi kama wataalam wa Afya ili kudhibiti ugonjwa wa homa ya nguruwe tunashauri kuzuia kabisa biashara ya nyama ya nguruwe kwa sababu ugonjwa huu hauna kinga’’,anasisitiza Chuwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa