• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HOSPITALI YA MKOA WA RUVUMA "HOMSO" YAPOKEA VIFAA VYA HUDUMA YA TIBA MTANDAO.

Tarehe ya kuwekwa: May 23rd, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

23 MEI 2022

Mganga Mkuu wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Ruvuma Dkt. Magafu Majura amepokea vifaa tiba mtandao kutoka Wizara ya Afya leo tarehe 23 Mei 2022.

Akizungumza wakati wa kupokea vifaa hivyo Dkt Majura alisema, vifaa hivyo vitatumika katika eneo la kupiga X-ray na Utra sound (Radiology) ambapo vipimo vitakavyofanyika vitaunganishwa katika mtandao na kwenda moja kwa moja katika Hospitali za kanda na Taifa.

Ameeleza kuwa lengo la kutumia vifaa hivyo ni kurahisha gharama za matibabu kwa kutuma majibu ya vipimo vya mgonjwa husika kabla ya kusafirishwa na kuwawezesha madaktari bingwa waliopo Hospitali za kanda na Taifa kutatua changamoto ya ugonjwa husika kwa njia ya mtandao.

Dkt Majura ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita kwa kuiwezesha Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Ruvuma kupata vifaa hivyo pamoja na kuleta fedha ambazo zimetumika katika ujenzi wa jengo la dharura pamoja na jengo la wagonjwa mahututi.

Mratibu wa huduma za tiba mtandao Wizara ya Afya Tanzania Dkt. Liggyle Vumilia amesema vifaa hivyo vimeletwa Mkoani Ruvuma kufuatia utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Mhe. Kassimu Majaliwa alipofika katika Hospitali hiyo mnamo Januari 5, 2019 kwa lengo la kuzindua X-ray ya kidigitali ambapo aliagiza Hospitali hiyo iungwe na huduma ya tiba mtandao.

Aliongeza kuwa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa hospitali nyingine nne zilizo pokea vifaa hivyo ikiwemo na hospitali za rufaa ya Mkoa wa Katavi,Tanga, hospitali za Wilaya ya Nzega na Chato ambapo vifaa vyote vimegharimu jumla ya Shilingi Billion 1 moja fedha ambazo zimetolewa na mfuko wa mawasiliano kwa wote (Universal communication Access Fund) kwa ajili ya ununuzi wa vifaa hivyo pamoja na gharama za uwekezaji.

Amebainisha kuwa jumla ya hospitali nyingine 16 za Mikoa zinatarajiwa kupelekewa vifaa hivyo kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma hasa kwa wananchi wanaoishi pembezoni kwa kupunguza gharama za kusafiri ili kupata huduma hizo.

Naye, Kaimu Mkuu wa kitengo cha mawasilino Serikalini Wizara ya Afya Catherine Sungura amesema kuwa Serikali ya Awamu ya 6 inaendelea kufanya maboresho katika sekta ya Afya nchini pamoja na kuhakikisha huduma za afya zinazotolewa kwa ubora na kwa wakati.

Amesema kuwa shilingi Million 630 zilitolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kisasa la wagonjwa wa dharura pamoja na shilingi Million 150 ya ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi ambapo majengo yote ujenzi umekamilika kwa asilimia 100% na yataanza kutumika hivi karibuni.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa