• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

IFAHAMU CHF ILIYOBORESHWA

Tarehe ya kuwekwa: September 7th, 2020

Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma Victor Nyenza ambaye pia ni  Mratibu wa Mfuko wa  Afya ya Jamii iliyoboreshwa iCHF amesimamia zoezi la utoaji  mafunzo kwa maafisa Waandikishaji 190 ambao wanatoka katika mitaa 95 iliyopo Manispaa ya Songea, iliyofanyika katika ukumbi wa  Ofisi ya kata Mfaranyaki Manispaa ya Songea 02/09/2020.

Nyenza alisema kuwa Mkoa wa Ruvuma una Maafisa Waandikishaji 1354, kutoka katika Halmashauri 8 nane ambao pia watapata  mafunzo haya ya Waandikishaji ambayo yataendelea kufanyika kwa nyakati tofauti  ndani ya Mkoa wa Ruvuma kama ilivyoelekezwa kwenye Waraka namba (1) wa maboresho ya Mfuko wa Afya wa jamii wa mwaka 2018.

Lengo kuu la mafunzo haya ni kuboresha utendaji wa kazi wa Afisa Mwandikishaji pamoja na uboreshaji wa mchakato mzima wa  usajili sahihi wa  wanachama  wa CHF ikiwa pamoja na ukusanyaji wa mapato kwa kutumia mfumo wa Kieletroniki na kuacha kutumia mfumo wa kawaida wa  malipo mkononi  ambao ulikuwa unasababisha upotevu wa fedha za Serikali.

Aliongeza kuwa lengo kuu la Mkoa wa Ruvuma ni kufanya  usajili kwa 50% ambapo hali halisi ya usajili Kimkoa  ni 3.6%,  Kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina lengo la kufanya usajili wa kaya 28820 sawa na 50% ambapo hali halisi ya usajili manispaa ya Songea ni 2.4% .

Alibainisha kuwa moja ya mkakati liyowekwa ni pamoja na kutoa mafunzo kwa Maafisa Waandikishaji wa mitaa/kijiji ndani ya Mkoa wa Ruvuma ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi bila ya upotevu wa mapato ya Serikali.

 Alifafanua kuwa CHF iliyoboreshwa inanufaisha  kaya yenye tegemezi 6 sita kama vile mkuu wa kaya, mwenza, na tegemezi wanne (4) wasiozidi miaka 18 kwa gharama ya shilingi elfu thelathini tu 30,000/= ambayo itatumika ndani ya mwaka mmoja.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

07.09.2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa