Halmashauri ya Manispaa ya Songea Katika Kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba 2022/2023 imepokea fedha jumla ya Tshs. 24,520,890,480.17 sawa na asilimia 52% ya fedha zilizotengwa shilingi 47,306,589,364 ambapo Kati ya fedha hizo, kiasi cha Tshs. 6,029,150,988.24 ni fedha za miradi ya maendeleo ambayo ni ujenzi wa madarasa 76 yenye thamani ya Tshs. 1,520,000.00 na ujenzi wa hospitali ya wilaya awamu ya pili kwa kiasi cha shilingi 500,000,000.
Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Manispaa ya Songea imekisia kukusanya kiasi cha shs 5,517,867,324.00 kutokana na vyanzo vya ndani vya mapato na hadi kufikia Disemba 2022 Halmashauri imekusanya kiasi cha shs 2,609,103,434.93 sawa na asilimia 47.2 ya lengo kwa mwaka ikiwa ni utekelezaji wa Ibara 122(c) ambayo inatutaka kuimarisha makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuimarisha makusanyo ya mapato katika vyanzo vilivyopo ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Hayo yamejili wakati wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa CCM wa mwaka 2020 kuanzia Julai hadi Disemba 2022 iliyofanyika tarehe 04 Februari katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ambayo yaliadhimishwa kuelekea kilele cha miaka 46 kuzaliwa kwa CCM tarehe 05/02 ambayo huadhimishwa kila mwaka.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya Songea Mjini Mwinyi Msolomi amewataka Viongozi mbalimbali kuacha Mipasuko ambayo itapelekea kuzorotesha shughuli za kimaendeleo.
Msolomi alisema lengo kuu la Serikali katika kuaajiri wataalamu ni kwa ajili ya kusimamia na kuratibu shughuli shughuli zote za Serikali pamoja na kusogeza huduma kwa wananchi,
Aliongeza kuwa katika kuelekea siku ya kilele cha maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM Miaka 46 ambapo kilele cha maadhimsho hayo yanafanyika Wilayani Tunduru, hata hivyo amewataka viongozi mbalimbali na wataalamu kuhakikisha wanapeleka wanafunzi waliochaguliwa kuijiunga kidato cha kwanza shule.
Kwa upande wake katibu wa CCM Wilaya ya Songea Mjini James Mgego alianza kwa kutoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa . Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Kusimamia na kuratibu maendeleo katika Sekta za miundombinu ya Barabara, madarasa, maji, umeme na Afya.
Mgego amewataka viongozi wa chama hicho ngazi ya Shina/ Tawi, Wilaya na Watendaji wa Serikali za Mitaa na Kata kuhakikisha wanatekeleza agizo lililotolewa kupitia kikao hicho la kufanya uhakiki wa wanafunzi wa kidato cha kwanza ambao bado hawajaripoti shule.
Ilani hiyo imesomwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea ambaye aliwakilishwa na Mkurugenzi Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko ambaye alisema Katika kutekeleza maelekezo ya Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 Halmashauri ya Songea ya Manispaa inatekeleza kazi mbalimbali za kiuchumi ambazo ni pamoja na Kilimo na biashara ambapo Kilimo huchangia asilimia 75 ya pato la Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambapo jumla ya Hekari 29,745.61 zimetengwa kwa ajili ya uwekezaji katika kata za Lilambo, Mwengemshindo, Tanga, Mletele na Ruhuwiko.
Dkt. Sagamiko alibainisha kuwa Katika kipindi cha Julai hadi Disemba 2022/2023 Jumla ya hekta 15,727.00 zimelimwa na matarajio ya mavuno ni tani 73,758.00 ambapo Kwa msimu wa mwaka 2022/2023 malengo ni kulima hekta 25,522.30 na matarajio ya mavuno ni tani 117,933.50.
Katika mwaka fedha wa fedha 2022/2023 Halmashauri imetenga 10% ya mapato ya ndani Kiasi cha Tshs 436,188,532.39 ambapo hadi kufikia mwezi Desemba 2022 jumla ya Tshs. 262,000,000.00 zimehamishwa kutoka akaunti ya makusanyo kwenda kwenye akaunti ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.
Alisema Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea inahudumia mtandao wa Barabara jumla ya kilometa 513.75 kati ya hizo, kilometa 256.69 ni za Mjazio (Feeder Roads, 254.99 ni za Mkusanyo (Collector Roads) na Kilometa 2.07 ni za Jamii (Community Roads) Barabara kwa ujumla katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea imegawanyika katika makundi makuu manne ambapo jumla ya kilomita 49.50 ni barabara za Changarawe , Kilomita 33.01 ni barabara za lami , kilomita 430.49 ni barabara za udongo na Kilomita 0.55 ni barabara za mawe pia kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Manispaa ya Songea imetengewa jumla ya TZS 2,571,280,000.00 kwa ajili ya kufanyia matengenezo mtandao wake wa barabara. “Dkt. Sagamiko, alibainisha”
Aliongeza kuwa Katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Disemba 2022/2023 Halmashauri ya Manispaa ya Songea imepokea fedha kiasi cha Tshs. 750,000,000.00 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa Hospitali ya Manispaa, Zahanati ya Makambi na ununuzi wa dawa, vifaa tiba na vitenganishi kwaajili ya vituo vya kutolea huduma za dawa.
Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ametoa Rai kwa watendaji wa kata na mitaa kushirikiana na wazazi kufanikisha kusimamia zoezi la wanafunzi wasioripoti shule na wale wote watakao kiuka taratibu hatua kali za kishria zitachukuliwa dhidi yao.
IMEANDALIWA NA;
AMINA PILLY;
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa