• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

JAMII INAHIMIZWA KWENDA KUPIGA KURA SIKU YA TAREHE 28 OKTOBA 2020

Tarehe ya kuwekwa: October 17th, 2020

Kwa kuzingatia kifungu cha 89A cha sheria ya Taifa ya uchaguzi sura 343 na kifungu cha 88A cha sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Sura 292, Tume haitasita kumchukulia hatua Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo/ Kata ambaye atasababisha makosa  ya  uchaguzi  kwa maksudi atachukuliwa hatua za  kisheria.  

Kauli hiyo imetolewa  na Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC) Dr. Wilson Charles akiwa katika kikao na Wasimamizi wa Uchaguzi Jimbo cha  kanda  kilichojumuisha mikoa sita yaani Mkoa wa Ruvuma, Mbeya, Njombe, Iringa, Lindi, na Mtwara kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea leo 17.10.2020.

Dr. Wilson alisema “ lengo kuu muhimu la kikao hicho ni kukumbushana masuala muhimu ya yatakayosaidia kuendesha vizuri zoezi la uchaguzi  Mkuu ambao unatarajia kufanyika tarehe 28 oktoba mwaka huu  kama ambavyo ilivyokuwa ikifanyika katika mazoezi mengine yanayopelekea  kukutana pamoja.  Aliongeza kuwa mkutano huo umeandaliwa kwa kanda sita ili kuwapunguzia umbali wa kusafiri kutoka kwenye maeneo yao na kuokoa muda katika kipindi hiki cha maandalizi ya Uchaguzi.

Alisema matarajio ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni kuwa na wasimamizi ambao watakuwa wameelewa vizuri maelekezo yote yaliyotolewa na Tume na kuweza kufanikisha kusimamia  zoezi la uchaguzi wa udiwani, Ubunge, na Rais.

Alibainisha kuwa baada ya kukamilika zoezi la uandikishaji daftari la wapiga kura lenye jumla ya wapiga kura  29,188,347 na  kwa upande wa Zanzibar jumla ya wapiga 566,352 wameandikishwa. Pia katika uchaguzi mkuu mwaka huu kutakuwa na jumla ya vituo 81,568 ikiwa  Tanzania bara kutakuwa na  jumla ya vituo 80,155 na Tanzania Visiwani jumla ya vituo 1413.

Alisema ongezeko hilo ukilinganisha na mwaka 2015 kulikuwa na jumla ya wapiga kura 23,166,144 na kufanya kuwa na ongezeko 6,000,000  la wapiga kura.  Alifafanua kuwa kila kituo kitakuwa na wapiga kura wasiozidi 450-500, pia  akinamama wajawazito, wenye watoto wadogo, wazee, na walemavu watapewa kipaumbele.

Aidha, kutakuwepo na vituo vya wazi kwa kuzingatia maelekezo ya Tume pia ujenzi wa vituo kwa kuzingatia idadi ya mawakala pamoja na kuweka eneo la  kitutuli ili mpiga kura aweze kupiga kura kwa uhuru na kwa haki.

Alisisitiza kutumia majengo ya umma kama shule, zahanati, na ofisi za kata ili kutunzia vifaa vya uchaguzi na kuhakikisha uwepo wa usalama wa vifaa pamoja na ulinzi wa eneo husika. Alisisitiza.

Dr. Wilson  aliwaasa wasimamizi wa Uchaguzi kubandika mabango ya mshale makubwa na madogo ili mpiga kura aweze kuona kituo kirahisi.

Alisema vituo vyote vinatakiwa kufunguliwa saa moja kamili 1:00 asubuhi bila kusahau sheria ya uchaguzi inakutaka ukishapiga kura unatakiwa kuondoka kituoni.

 IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

  

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa