• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

JIUNGE NA SACCOS YA MANISPAA BORESHA MAISHA YAKO.

Tarehe ya kuwekwa: December 26th, 2020

CHAMA cha akiba na mikopo SACCOS Manispaa ya  Songea kilianzishwa januari 1988 na kuandikishwa rasmi Aprili 1988 kwa namba RVR 153 kikiwa na wanachama 20, lakini idadi hiyo imeendelea kuongezeka hadi sasa kufikia idadi ya wanachama 288 me 110 na ke 178 licha ya wanachama wengine kujiondoa kutokana na sababu ya kifo, kustaafu, kuhama, na matatizo ya kiuchumi.

Hayo yamebainika katika mkutano wa kawaida wa 28 wa chama cha akiba na mikopo SACCOS uliofanyika katika ukumbi wa St.Augustine uliopo Manispaa ya Songea leo tarehe 26.12.2020.

Mgeni rasmi katika Mkutano huo alikuwa  Meneja wa  Biashara  na Mahusiano  NMB tawi la Songea Augustino Manguya ambaye alianza  kwa kutoa pongezi  kwa viongozi  wote ambao wamemaliza muda wao wa  uongozi kwa muda wa miaka mitatu kwa uendeshaji  mzuri wa chama.” Aliwapongeza.

Manguya aliwataka wanachama wote kukopa chamani  sambmba na kuanzisha au kuboresha miradi yao  ili kujiongezea kipato , pamoja nakufanya  marejesho  ya mikopo ili kuzidi kuimarisha chama na kuwa mkopaji bora kwa kufanya hivyo Chama kitaweza kukua kimtaji.

Naye  Katibu wa chama cha SACCOS Winifrida Komba  aliweka bayana masharti ya chama hicho ambayo yanasema “ kifungu cha 41(2) g,  kinasema mkutano mkuu wa kawaida huthibitisha majina ya wanachama wapya na wanaojitoa na kuchukua hatua ya kinidhamu kwa baadhi ya  wanachama wanaokiuka masharti ya chama ambapo katika mkutano huo walithibitsha wanachama wapya 27 na kuwaondoa wanachama 19 waliokoma uanachama kwasababu mbalimbali ikiwemo kifo, kustaafu, kuhama, na matatizo ya   kiuchumi”

Naye mwenyekiti wa SACCOS Iddi Waziri ambaye amemaliza muda wake wa uongozi alisema mwaka 2019 chama kilikisia kukusanya shilingi 550,000,000/= hali halisi ya hadi disemba 2019 ilikusanywa shilingi 523,450,059.00 sawa na asilimia 95% ya lengo walilojiwekea sambamba na utoaji wa mikopo iliyotolewa kwa asilimia 93%.

Waziri alitanabaisha kuwa mwaka 2020 chama kiliweka makisio ya mapato shilingi 81,800,000/= kutokana na faida ya juu ya mkopo, viingilio, na mapato mengine na kuwa hali halisi ya makusanyo  shilingi 80, 870, 785.15 sawa na asilimia 98.8 ya makisio hadi disemba 2020, ikiwa na mafanikio ya kukopesha wanachama 208  yenye thamani ya shilingi  458, 650, 000/=  sawa na asilimia 109 ya lengo walilojiwekea.

Akitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili chama  hicho ni pamoja na  baadhi ya wanachama waliopewa mkopo kutorejesha mikopo kwa wakati  hali inayodhoofisha ufanisi wa chama na kuwa na mikopo chechefu isiyo na tija na kusababisha wanachama kushindwa kupatiwa mikopo kwa wakati, wanachama kukosa sifa ya kukopa kutokana baki ya moja ya tatu ya mshahara wake, baadhi ya marejesho ya mkononi kutorejeshwa kwa wakati,  baadhi ya wanachama kukatwa chini ya kiwango, wanachama wanaochangia akiba kwa fedha tathilimu kushindwa kuchangia kwa wakati na nyinginezo.

Ufumbuzi wa changamoto hizo ni pamoja na wadaiwa sugu kesi zao kupelekwa  TAKUKURU, wanachama wanaokatwa chini ya kiwango watoe ushirikiano ili kuweza kupewa taratibu za  kuongezea marejesho yanayokatwa chini ya kiwango,  wanachama wanaokosa moja ya tatu kuendelea kutumia utaratibu wa kutumia standing order ili waweze kuchangia chamani.

Alisema mnamo tarehe 09 julai 2020 bodi ilimsimamisha kazi  Frola Luoga kwa makosa ya utovu wa nidhamu na kukosa uaminifu  katika utendaji wake wa kazi na kuisababishia  chama hasara ya kiasi cha fedha shilingi 4,847,101.75 pamoja na  kushindwa kuwasilisha risiti  ya makato ya watumishi  NSSF kwa wakati na chini ya kiwango. Kutokana na kusimamishwa kwa kazi kwa Flora  Luoga, chama kitatangaza nafasi hiyo kwa kufuata taratibu za ajira.

 Mwisho alisema uchaguzi wa viongozi wapya ni sheria ya ushirika yamwaka 2015 ya kanuni za SACCOS  2018, ya masharti ya chama sehemu namba 48 na kifungu cha 4, inawaambia wanachama kuchagua viongozi bora wenye weredi watakaokiongoza chama kwa muda wa miaka mitatu ijayo.

Baada ya kusema hayo Afisa ushirika Given Mariki alitangaza matokeo ya uchaguzi wa wajumbe wa bodi pamoja Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti ambapo matokeo ya uchaguzi huo ndugu Amiri Ayuob alichaguliwa kuwa mwenyekiti aliyepita bila kupingwa, na makamu mwenyekiti Zacharia Kapinga alipata kura 158  dhidi ya mpinzani wake Bakari kawina aliyepata kura 26.

Mwisho mwenyekiti mteule Amiri Ayoub aliwashukuru wanachama kwakumchagua na kuomba ushirikiano kwa wanachama  wote waliomchagua.

 IMETYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

26 Disemba 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa