• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.

Tarehe ya kuwekwa: January 19th, 2023

Kamati ya fedha na Uongozi Manispaa ya Songea imefanya ziara ya kutembelea miradi ya Maendeleo kwa lengo la kufanya ukaguzi wa miradi inayotekelezwa katika Halmashauri na kuthaminisha hali ya mradi na thamani ya fedha iliyotolewa.

Kamati hiyo iliongozwa na Mstahiki Meya Manispaa ya Songea  Michael Mbano iliyofanyika jana tarehe 18 Januari 2023 na kufanikiwa kutembelea miradi  wa ujenzi wa uzio wa Bweni la watoto wenye mahitaji maalmu kata ya Subira kwa fedha Mil.  60  kutoka Serikali kuu, ukamilishaji wa Bweni Sekondari ya Chabruma kata ya Lilambo kwa fedha Mil 22 kutoka Serikali kuu, ukamilishaji wa madarasa mawili Shule ya Msingi Sabasaba fedha Mil. 25 kutoka Serikali kuu, kukagua miradi ya barabara za mitaa za  kata ya Bombambili na Msamala  kwa  thamani ya Mil. 20,000  kwa kila kata fedha za mapato ya ndani, Ukamilishaji wa Bweni Mdandamo Sekondari kwa fedha Mil 38 kutoka Serikali kuu pamoja na kukagua mradi wa kivuko kata ya Mletele Mil 20 kwa fedha za  mapato ya ndani.

Mhe.Mbano alianza kwa kuwapongeza wataalamu kwa kutoa fedha mil. 20 fedha za mapato ya ndani  kupeleka kwenye  kila Kata kwa ajili ya kutekeleza miradi  mbalimbali ambayo imekuwa ni adha katika kata husika ambapo katika kutekeleza agizo hilo kata 3 za awali  ambazo ni kata ya   Bombambili, kata ya Msamala, na Mletele zimeshapokea fedha hizo na utekelezaji wa kazi umeshakamilika.  “Amepongeza“

Alibainisha kuwa kata ya Bombambili imepokea fedha Mil 20 imetumika kutengeneza barabara za mitaa, kata ya Msamala imepokea fedha Mil. 20 ambazo zimetumika kwa ajili ya utengenezaji wa kivuko  Mtaa wa Mtaungana ambapo  imesaidia kutatua changamoto ya kivuko kuelekea Kata ya Mjimwema na  ujenzi wa kivuko kata ya Mletele. “ Mhe. Mbano alibainisha.”

Hata hivyo kamati ya fedha na uongozi ilipongeza jitihada za wataalamu kwa kusimamia vizuri miradi ya maendeleo ambapo wametoa rai kwa wataalamu kuendelea kutoa ushirikiano katika kusimamia na kutekeleza miradi ya maendeleo ya Halmashauri.

Akitoa shukrani kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na  Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro kwa kutoa fedha za miradi mbalimbali ambayo inaendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea ikiwemo na fedha za  ujenzi wa madarasa  76 ambayo kwasasa yamekamilika na watoto wameingia darsani. "Mstahiki Meya alishukuru".

Kwa upande wake Afisa Mtendaji kata ya  Msamala Deogratias Chaima  alisema kuwa katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023 kata ya Msamala imepokea shilingi Mil. 20 kutoka kwa Mkurugenzi Manispaa ya Songea fedha za mapato ya ndani ambazo zimetumika kutengeneza kivuko na bara bara za mitaa KM. 7.9.

Imeandaliwa na;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

 

 



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa