• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI ya Fedha yakagua miradi ya maendeleo

Tarehe ya kuwekwa: February 2nd, 2018

KAMATI ya Fedha na Uongozi ya ya Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Songea imefanya ziara ya kukagua miradi iliyotekelezwa katika robo ya pili.

Miradi iliyokaguliwa ni ujenzi wa machinjio ya kisasa katika kata ya shule ya Tanga unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni tatu ambao umefikia asilimia 40 ya ujenzi.Mradi huo unatarajia kukamilika Juni 2018.

Miradi mingine ni ujenzi wa madarasa matano na matundu 12 ya vyoo katika shule ya msingi Majimaji unaogharimu milioni 66.6 na mradi wa ujenzi wa madarasa matano na matundu 12 ya vyoo katika shule ya msingi Kipera ambao unaogharimu milioni 61.

Kamati imeridhishwa na ujenzi wa Miradi yote isipokuwa katika mradi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Changarawe kata ya Mletele ambapo hali ya ujenzi hairidhishi wanafunzi wanasomea katika madarasa ambayo hayana sakafu na wengine wanasomea chini ya Miti.

Mchumi Mkuu wa Manispaa ya Songea Kimary amesema Manispaa kupitia mapato ya ndani imetoa shilingi milioni 22 kwa ajili ya ujenzi wa matundu 12 ya vyoo na vyumba viwili vya madarasa ambavyo ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 60.

Amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2017/2018 kupitia mapato ya ndani Halmashauri ya Manispaa ya Songea imetenga shilingi milioni 127 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo katika shule 12 ikiwemo na shule ya msingi Changarawe.

Kamati imeagiza marebisho yafanyike haraka katika shule ya msingi Changarawe ili watoto wasiendelee kusomea nje kwa kuwa hali hiyo inaitia haibu Manispaa ya Songea.

Takwimu zilizotolewa na Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema wakati anazungumza na madiwani wa Manispaa ya Songea hivi karibuni zinaonesha kuwa Manispaa ya Songea inakabiliwa na upungufu wa vyumba 500 vya madarasa kwa shule za msingi.

Sera ya elimu bure imepata mafanikio makubwa ya kuandikisha idadi kubwa ya wanafunzi hali inayoleta Changamoto katika vyumba vya madarasa katika shule za msingi na sekondari.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa