• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA SIASA SONGEA MJINI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Tarehe ya kuwekwa: September 13th, 2022

Kamati ya Siasa Wilaya ya  Songea  Mjini (CCM) imeridhishwa na utendaji wa kazi wa miradi maendeleo  inayoendelea kujengwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea  kutokana na miradi hiyo kutekelezwa kwa kiwango kizuri.

Ziara hiyo imefanyika leo 13 Septemba 2022 iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Songea Mjini  Hamisi Abdallah Ally ambaye  ametembelea miradi mbambali ya maendeleo iliyopo kwenye kata ambapo aliongozana na  wajumbe wa kamati ya siasa Wilaya, na Wataalamu kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa kituo cha afya Lilambo kilichojengwa kwa shilingi Mil.500 fedha za mapato ya ndani, ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya Ruhila iliyopo kata ya Mshangano iliyojengwa kwa shilingi Mil. 470 fedha za mradi wa SEQUIP shule ambayo tayari imefunguliwa rasmi tarehe 05 septemba 2022 na kuanza rasmi msimu wa masomo kwa wananfunzi.




Aidha, walitembelea pia  Ujenzi wa kituo cha afya Mletele uliyopo katika kata ya Mletele unaojengwa kwa kwa gharama ya shilingi mil. 545,334,640 fedha kutoka Global fund, ujenzi wa mabweni 4, madarasa 3 kwa shilingi Mil 260 uliyopo shule ya wavulana Songea katika kata ya Seedfarm ukiwa hatua ya kupaua,   pamoja na ujenzi wa mabweni 4, na madarasa 3 matatu katika shule ya wasichana Songea kwa gharama ya shilingi Mil. 280 uliopo katika kata ya Mjini.

Hamisi amewapongeza wataalamu wote kwa usimamizi thabiti wa miradi ya maendeleo na amewataka kutatua changamoto ndogondogo  zinazojitokeza katika utekeleza  miradi hiyo na  kukamilisha kwa wakati .

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa kituo cha Afya Lilambo  Afisa Mtendaji wa Kata ya Lilambo Teah Komba alisema bajeti ya mwaka 2021/2022 mradi  uliidhinishiwa kiasi cha fedha Mil 500 kutoka mapato ya ndani pamoja na nguvu za  wananchi wakiwa wamechangia kiasi cha shilingi 3,295,000  ambapo hadi hivi sasa upo hatua ya ukamilishaji.

Aidha Mkuu wa shule ya Sekondari ya Wavulana Songea  Gelasius Lugome alisema mradi huo uliibuliwa na Serikali mwaka 2022  na kutekelezwa kupitia SEQUIP ambao umelenga kunufaisha shule kwa kuongeza madarasa matatu 3 na mabweni 2 mawili kwa lengo la kuongeza udahili wa  wanafunzi wa kidato cha tano na kupunguza msongamano mabwenini na madarasani.

Lugome amebainisha kuwa mradi huo unatekelezwa kwa mfumo wa “FORCE ACCOUNT “kama ilivyoamuliwa na Serikali ambapo kwasasa upo hatua ya upauaji kwa mabweni na ujenzi wa madarasa hatua ya ukamilishaji.

Wajumbe wakamati ya siasa wakitoa maoni yao kwa pamoja wameonesha kuridhishwa na mwenendo wa utekelezaji wa miradi yote iliyotembelewa na wamewarai  wataalamu kutekeleza miradi hiyo kwa kufauata taratibu za manunuzi zilizowekwa na Serikali.

IMEANDAILIWA NA;

AMINA PILLY

AFISA HABARI.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa