• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI ya Ulinzi na Usalama yatembelea machinjio ya kisasa

Tarehe ya kuwekwa: April 6th, 2018

KAMATI ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Songea ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema imekagua mradi wa machinjio ya kisasa unaotekelezwa katika Kata ya Tanga Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kamati hiyo kabla ya kuanza ukaguzi,Kaimu Mhandisi wa Ujenzi wa Manispaa ya Songea Mhandisi Nicolus Danda amesema mradi wa machinjio ya kisasa unafadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya shilingi zaidi ya bilioni tatu.

Amemtaja Mkandarasi wa mradi huo ambaye hadi sasa amelipwa shilingi milioni 400 kuwa ni Kampuni ya Giraffe ambapo mkataba wake ni  wa mwaka mmoja ambao   umeanzia Julai 2017 na kukamilika Juni 30, 2018.

Kwa mujibu wa Danda kazi ambazo zinafanyika kwenye mradi huo ni ujenzi wa machinjio yenye urefu wa meta 64 na upana wa meta 24,ujenzi wa zizi lenye uwezo wa kuhifadhia ng’ombe 200 na ujenzi wa uzio,tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita ya 162,000.

Kazi nyingine anazitaja kuwa ujenzi wa nyumba mbili ikiwemo ya daktari wa mifugo na mlinzi,ujenzi wa barabara ya kilometa moja ambayo itazunguka eneo  la mradi na ujenzi  wa maeneo ya kupaki magari.

Mkandarasi huyo ameahidi kumaliza kazi ndani ya mkataba ambapo amesema hivi sasa imebakia mistari michache kukamilisha kuzungusha jengo lote kisha kuanza kazi ya kjkamilisha maeneo yaliobakia pamoja na kuezeka machinjio.

Akizungumza mara baada ya ukaguzi wa mradi huo Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema ameridhishwa na viwango vya ujenzi wa machinjio hiyo,hata hivyo ameshauri kuangaliwa upya viwango vya fedha ambazo zinatolewa  kwa maoni yake anaona ni fedha nyingi ukilinganisha na kazi ambazo zinafanyika kwenye mradi husika.

Hata hivyo Mgema amempongeza Mkandarasi huyo kwa kazi kubwa ambayo ameifanya ukilinganisha na kiwango cha fedha cha shilingi milioni 400 ambazo ni malipo ya awali ambazo amelipwa hadi sasa na Manispaa ya Songea.

Wawakilishi toka Benki ya Dunia mwezi Machi mwaka huu wamefanya ukaguzi katika mradi huo na kuridhishwa na viwango vya ujenzi wa mradi huo.

Kamati ya Fedha na Uongozi ya Baraza la Madiwani la Manispaa ya Songea,tayari imekagua mradi huo na kuridhishwa na kazi ya Mkandarasi huyo.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Aprili 6,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa