• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMPENI ya Mwanamke kumilikishwa ardhi

Tarehe ya kuwekwa: November 10th, 2019

TANZANIA imechaguliwa na Umoja wa Mataifa kuwa nchi ya kwanza kufanya kampeni ya kuhakikisha mwanamke anapata haki ya kumiliki ardhi kama ilivyo kwa wanaume.

Kampeni hii ni endelevu inafanyika kwa miaka 12 kuanzia  mwaka 2019 hadi 2030 na inatarajiwa kuzinduliwa Novemba 21,2019 jijini Dar es salaam na Waziri wa Afya,Jinsia,Maendeleo ya Jamii,wazee na watoto Ummy Mwalimu.

Wadau 25 kutoka Taasisi mbalimbali wanashiriki katika kampeni hii  likiwemo Shirika la kimataifa la Landesa ambalo ni Taasisi inayoshughulikia maendeleo vijijini na wanahabari ambao watasaidia kufanikisha kampeni hii kuwafikia watu wengi.

Godfrey Massay ni Mwanasheria na Mtaalam wa masuala ya ardhi kutoka Taasisi ya Landesi anasema Tanzania ina sera na sheria bora za ardhi ambazo zinakabiliwa na changamoto katika utekelezaji wake hivyo kusababisha baadhi ya watu kama wanawake kukosa haki za kumiliki ardhi .

“Tanzania imechaguliwa kuwa ya kwanza na Umoja wa mataifa kuona namna ya kuwasaidia  wanawake kumiliki ardhi kwa sababu,ardhi ni maisha na kila kitu,sera na sheria nzuri zilizopo zinatakiwa zitekelezeke’’,anasisitiza Massay.

Hata hivyo anaitaja sababu ya Tanzania kuchaguliwa kuwa nchi ya kwanza kutekeleza kampeni hii kuwa ni kutokana na utashi wa serikali uliopo na kampeni zilizofanyika siku za nyuma  kama Mama Ardhi kupata mafanikio makubwa.

Akizungumza wakati anatoa mafunzo maalum kwa wanahabari takribani 20 waliochaguliwa katika nchi nzima kujifunza habari zinazohusiana na haki ya mwanamke katika ardhi na uwekezaji wajibifu,Massay anasema mafunzo hayo yanatolewa kwa wanahabari kwa sababu wana namna nyingi za kufikisha ujumbe katika jamii.

Anasisitiza kuwa wakati sasa umefika duniani kote  kuhakikisha mwanamke anapata haki ya kumiliki ardhi na kwamba hapa Tanzania kuanzia Katiba ya nchi ya mwaka 1977 hadi sheria  ya ardhi ya mwaka 1999 kifungu cha nne na tano  vinampa nafasi mwanamke kumiliki ardhi.

Imeandikwa na Albano Midelo,Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa